MAKANGALESOPHIE

  • Subscribe to our RSS feed.
  • Twitter
  • StumbleUpon
  • Reddit
  • Facebook
  • Digg

Wednesday, 12 December 2012

Pembe, Meno ya tembo ni biashara ya nani?

Posted on 23:29 by Unknown

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Iringa, Michael Kamuhanda (Kushoto) akizungumza na Waandishi wa habari alipokuwa akiwaonesha meno ya Tembo yaliyokamatwa juzi Mkoani humo. (Picha : Geofey Nyang'oro/Mwananchi)

KWA mara nyingine katika muda usiozidi wiki tatu, watu watatu wametiwa mbaroni kwa kosa la kusafirisha pembe 78 za ndovu kutoka wilayani Masasi, mkoani Mtwara. Tunaambiwa kuwa, Pembe hizo ambazo wataalamu wa wanyamapori wanasema zimetokana na tembo 39 zimekadiriwa kuwa na thamani ya Sh935 milioni.

Polisi wanasema askari waliokuwa katika moja ya vituo vya ukaguzi mjini Iringa walilisimamisha gari hilo lililokuwa na shehena ya pembe hizo za ndovu mapema wiki hii baada ya kulishtukia, lakini dereva wa gari hilo alikataa kusimama, hivyo kuwalazimisha askari katika kituo hicho cha ukaguzi kulifukuza gari hilo na kufanikiwa kulikamata katika Kituo cha Polisi cha Ruaha Mbuyuni ambapo polisi walikuwa wameweka kizuizi baada ya awali kupewa taarifa na wenzao wa mjini Iringa.

Mshikemshike na kashkashi iliyotokea katika kituo hicho cha Polisi mpaka majangili hayo yakatiwa mbaroni ilikuwa kubwa ingawa sasa ni historia. Hata hivyo, yafaa ifahamike tu hapa kwamba majangili hayo yalilitekeleza gari hilo lenye shehena na kujificha vichakani hadi wananchi walipoyakurupusha na kuwawezesha polisi kuyakamata pamoja na gari hilo lenye pembe hizo za ndovu zenye uzito wa kilo 212.

Tumezungumzia sakata hilo kwa kirefu kutokana na ukweli kuwa, kwa muda mrefu sasa matukio ya vitendo vya ujangili wa kutisha katika mbuga zetu za wanyama vimekuwa vya kawaida. Ilifika wakati majangili wakapata ujasiri wa ajabu wa kuwakamata wanyama mchana kweupe, wakiwamo twiga, na kuwasafirisha nje ya nchi kupitia katika viwanja vyetu vya ndege ambavyo vina ulinzi mkubwa pengine kuliko mahali popote hapa nchini.

Tukio hilo ambalo hakika lilikuwa la aina yake tangu nchi yetu ipate uhuru liliiacha Serikali katika aibu na mfadhaiko mkubwa, kwani lilionyesha pasipo shaka kwamba nchi yetu ina mtandao mkubwa wa ujangili unaohusisha baadhi ya wafanyabiashara wakubwa, wanasiasa, vigogo serikalini na baadhi ya watumishi katika vyombo vya ulinzi na usalama.

Vitendo hivyo vya ujangili na usafirishaji nje wa pembe za ndovu na nyaraka nyingine za Serikali umeiacha nchi yetu katika aibu kubwa. Mwezi uliopita, Serikali ilikiri kukamatwa nchini China kwa pembe 569 za ndovu zenye thamani ya Sh2.24 bilioni kutoka Tanzania.

Hii ilitanguliwa na matukio mengi ya aina hiyo ambayo hakika yameifanya Tanzania kuonekana kituko mbele ya Jumuiya ya Kimataifa.

Wengi wanajiuliza, biashara ya pembe za ndovu inamilikiwa na kuwezeshwa na kina nani? Usafirishaji wa pembe hizo na nyaraka nyingine unaratibiwa na magenge gani katika bandari, stesheni za treni na viwanja vya ndege? Ni kwa kiasi gani vyombo vya kiserikali kama Jeshi la Polisi, Usalama wa Taifa na Mamlaka ya Mapato Nchini (TRA), vinahusika?

Hayo bila shaka ni maswali magumu yanayohitaji majibu. Haiwezekani nchi yetu iendelee kuporwa rasilimali zake, huku mamlaka husika zikitazama tu pasipo kuchukua hatua stahiki na kuwaacha wananchi wakiogelea katika umaskini wa kutisha. Pamoja na hatua za zimamoto zinazochukuliwa hivi sasa na wizara husika, ukweli ni kuwa, kwa muda mrefu Serikali imekosa utashi wa kisiasa wa kukomesha vitendo hivyo au kufanya ufuatiliaji wa namna fulani.

Ndiyo maana wengi wanadhani Serikali inajua kinachoendelea. Inakuwaje mamia ya watu wanaokamatwa kwa ujangili au usafirishaji wa nyara za Serikali hawabanwi vya kutosha ili wawataje wamiliki wa biashara hiyo au mawakala wao?

via gazeti la Mwananchi







































































Email ThisBlogThis!Share to XShare to FacebookShare to Pinterest
Posted in Local News | No comments
Newer Post Older Post Home
View mobile version

0 comments:

Post a Comment

Subscribe to: Post Comments (Atom)

Popular Posts

  • Christiano Ronaldo and His 29 girlfriends List.
    Chr is tiano Ronaldo is famous as a great and cool football player. He play for England Manchester United Club, at age of 26 and he already...
  • Maadhimisho ya miaka 100 ya kituo cha makumbusho ya utamaduni wa Kisukuma - BUJORA Mwanza.
    Maadhimisho ya miaka 100 ya kituo cha makumbusho ya utamaduni wa Kisukuma - BUJORA Mwanza.                 Makumbusho ya  ka...
  • Tumehuzunika kidogo, Cesc Fabregas
  • Computer System Analyst Grade I (Business Analysis) – One Post - (Re-advertised) E-Government Agency (EGA
    Computer System Analyst Grade I (Business Analysis) – One Post - (Re-advertised) E-Government Agency (EGA) Date Listed: J...
  • Post: Part-time journalist
    Post: Part-time journalist Job Description Timely and accurately collecting African real-time news and then integrate the manuscript ...
  • Tempetation
    An Ivy League-educated marriage counselor who gives marital advice but finds it difficult to address issues with her own marriage.    Jur...
  • University of Dar es Salaam among top 100 Universities in Africa
    The university of Dar-es-Salaam has ranked fourth among top 100 popular universities and higher learning institutions in Africa. This is acc...
  • Admission of Diploma holders into Higher
    TANZANIA COMMISSION FOR UNIVERSITIES Admission of Diploma holders into Higher Education Institutions for the academic year 2013/2014. The T...
  • Community Relations Manager – (One Post)
    Community Relations Manager – (One Post) African Barrick Gold (ABG) Date Listed: May 15, 2013 Email Address: ...
  • Kim Kardashian awateka tena mashabiki kwa mavazi
    Kim Kardashian aliweza tena kuuteka umati waliohudhuria katika sherehe za kuchangisha fedha kwa ajili ya mfuko wa kuchangisha fedha kwa ajil...

Categories

  • Africa (1)
  • Announcement (13)
  • Biashara (17)
  • Breaking News (4)
  • Burudani (11)
  • East Africa News (19)
  • Education (12)
  • Entertainment (8)
  • Fashions (1)
  • Habari (41)
  • Health (1)
  • International News (14)
  • Jamii (11)
  • Jobs (120)
  • Latest Sports News (3)
  • Local News (59)
  • Makala (8)
  • Michezo (25)
  • Music (5)
  • News (12)
  • Scholarships (4)
  • Scholarships- Jobs (7)
  • Siasa (1)
  • Sport (64)
  • sports (18)
  • Technology (2)
  • Tetesi za Usajili (9)
  • usajili (1)

Blog Archive

  • ►  2013 (335)
    • ►  September (9)
    • ►  August (18)
    • ►  July (23)
    • ►  June (27)
    • ►  May (91)
    • ►  April (53)
    • ►  March (41)
    • ►  February (59)
    • ►  January (14)
  • ▼  2012 (162)
    • ▼  December (42)
      • Reduce burden on workers
      • Challenges facing small holder farmers in Mvomero ...
      • Wakurugenzi wengine 16 wa Bandari wasimamishwa kazi
      • Fight against Ebola in SADC and East African Region
      • leave the issue of tax administration in the hands...
      • The increasing challenge on human trafficking and ...
      • Manchester United’s Christmas bash....
      • Pembe, Meno ya tembo ni biashara ya nani?
      • BENKI ya Taifa ya Biashara (NBC) kudhamini Vijana...
      • NBC VOWS ETERNAL LOVE TO SMEs
      • "FAIR SHARES FOR WORKERS IS THE CRY"
      • GOVERNMENT TO ESTABLISH YOUTH BANK .
      • Government has set Tshs 1.5 Billion for Youth.
      • DCB has opened more two Branches in Dar es Salaam.
      • Robin van Persie Amazing Free Kick Goal Manchester...
      • Job Description: Manager, Policy & Partnership
      • BEN ARFA AMAZING GOAL Fulham (2-1) Newcastle Unite...
      • Man with 'bionic' leg to climb 103 Floors of Chica...
      • Football's Greatest - Gerhard "Gerd" Müller (2010)...
      • Pamoja na ukali wake huyu dogo alikuwa analipwa T ...
      • Project Leader - Serengeti National Park, Tanzania
      • 1st Line Support Engineer-Vacancy
      • The East African's News Round Up
      • SPOTLIGHT ON CHILDREN'S NEEDS
      • Barclays Bank Tanzania has Announced winner of the...
      • How to generates great wealth!!!
      • Tumetoka mbali na simu za mikononi...
      • Arsene Wenger aomba dua la kutokupangwa na Barcelona
      • Pesa si ushindi, Man City yadunda hata kutinga Eu...
      • Research Consultant (International Development Res...
      • Master Jury Announced for 2013 Aga Khan Award for ...
      • Jose Mourinho anaweza kuingoza Manchester United
      • Commonwealth Distance Learning Scholarships 2012-2...
      • FIND your scholarships and grants to study in Europe!
      • Introduction to DAAD Scholarships
      • DAAD-Undergraduate Scholarship
      • Scholarship Program
      • News in brief.....Habari Mchanganyiko
      • Ratiba ya kombe la FA mzunguko wa Tatu yatoka
      • Matokeo ya Michezo ya Premier Ligi katika picha mi...
      • RAFA BENITEZ Akalia kuti kavu
      • Timu ya Beckham yanyanyua tena ubingwa kwa mwaka w...
    • ►  November (70)
    • ►  October (50)
Powered by Blogger.

About Me

Unknown
View my complete profile