MAKANGALESOPHIE

  • Subscribe to our RSS feed.
  • Twitter
  • StumbleUpon
  • Reddit
  • Facebook
  • Digg

Wednesday, 3 July 2013

Mabilionea Tanzania wakutana na Obama

Posted on 05:45 by Unknown
Dar es Salaam. Rais wa Marekani, Barack Obama juzi alikutana na kundi la wafanyabiashara 20 wakubwa barani Afrika wakiwemo Watanzania watatu ambao utajiri wao ulitajwa katika jarida la Ventures Africa linalozungumzia masuala mbalimbali ya uchumi wa Afrika, kuwa ndiyo matajiri zaidi nchini.

Tumezungumza mengi na Obama, ila ulikuwa mkutano wa ndani na mrefu, tumezungumza mengi kwa kweli.’ Reginald Mengi, Mkurugenzi Mtendaji wa IPP
Obama ambaye ni Rais wa 44 wa Marekani alikutana na wafanyabiashara hao juzi jioni katika Hoteli ya Hyatt Kilimanjaro na kufanya nao mazungumzo kwa saa 1:23, huku waandishi wa habari wakipewa ruhusa ya kupiga picha tu.
Jarida hilo lililotolewa mwaka jana liliwataja wafanyabiashara hao kuwa ni Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Bakhresa Group, Said Salim Bakhresa, Gulam Dewji, Rostam Aziz, Mwenyekiti Mtendaji wa Kampuni ya IPP, Reginald Mengi na Mwanzilishi na Mwenyekiti Mtendaji wa Tanzania Infotech Investment Group, Ali Mufuruki.
Hata hivyo, juzi wafanyabiashara waliokuwa katika orodha ya kukutana na Rais Obama ni Bakhressa, Mengi na Mufuruki.
Anayeongoza katika orodha hiyo ni Bakhressa anayemiliki mali na fedha zenye thamani ya Dola za Marekani 620 milioni sawa na Sh992 bilioni (Dola moja Sh1,600) akifuatiwa na Dewji ambaye utajiri wake ni Dola 560 milioni (Sh896 bilioni).
Wengine na kiasi cha mali na fedha wanazomiliki kwenye mabano ni Rostam (Sh672 bilioni- Dola 420 milioni) Mengi (Sh448bilioni- Dola 280 milioni) na Mufuruki (Sh176 bilioni - Dola 110 milioni).
Mara baada ya kumalizika kwa kikao hicho, Rais Obama alizungumza tena na wafanyabiashara wengine 170 kutoka Afrika na Tanzania kwa dakika 17, lakini hakuweka wazi walichozungumza na wafanyabiashara hao 20.
Wafanyabiashara wengine waliokuwepo katika kikao hicho ni pamoja na Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Africa Finance Corporation, Andwer Alli, Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya Maendeleo Afrika, Don Kaberuka..
Wengine ni Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), Dk Richard Sezibera, Mwenyekiti wa Econet, Strive Masiyiwa, Mkurugenzi Mkuu wa Equity Benki, James Mwangi, Mwenyekiti wa Export Trading Group, Mahesh Patel.
Mkurugenzi Mkuu wa General Electric, Jay Ireland, Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Harith, Tshepo Mahloele, Mwenyekiti wa Heirs Holdings, Tony Elumelu.
Makamu wa Rais wa Kampuni ya Microsoft Afrika, Ali Faramawy, Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Prudential Plc, Tidjane Thiam, Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Standard Chartered, Peter Sands, Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Symbion Power, Paul Hinks, Mwanzilishi na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Tanjet, Susan Mashibe pamoja na Mwenyekiti wa Benki ya United Afrika, Phillips Oduoza.
Katika meza kuu Obama alikuwa amekaa pamoja na Mashibe, Mahloele, Masiyiwa na Kalumbu.

Habari kwa msaada wa gazeti la mwananchihttp://www.mwananchi.co.tz/habari/Kitaifa/Mabilionea-Tanzania-wakutana-na-Obama/-/1597296/1902762/-/qp050rz/-/index.html
Email ThisBlogThis!Share to XShare to FacebookShare to Pinterest
Posted in Local News | No comments
Newer Post Older Post Home
View mobile version

0 comments:

Post a Comment

Subscribe to: Post Comments (Atom)

Popular Posts

  • Christiano Ronaldo and His 29 girlfriends List.
    Chr is tiano Ronaldo is famous as a great and cool football player. He play for England Manchester United Club, at age of 26 and he already...
  • Maadhimisho ya miaka 100 ya kituo cha makumbusho ya utamaduni wa Kisukuma - BUJORA Mwanza.
    Maadhimisho ya miaka 100 ya kituo cha makumbusho ya utamaduni wa Kisukuma - BUJORA Mwanza.                 Makumbusho ya  ka...
  • Tumehuzunika kidogo, Cesc Fabregas
  • Computer System Analyst Grade I (Business Analysis) – One Post - (Re-advertised) E-Government Agency (EGA
    Computer System Analyst Grade I (Business Analysis) – One Post - (Re-advertised) E-Government Agency (EGA) Date Listed: J...
  • Post: Part-time journalist
    Post: Part-time journalist Job Description Timely and accurately collecting African real-time news and then integrate the manuscript ...
  • Tempetation
    An Ivy League-educated marriage counselor who gives marital advice but finds it difficult to address issues with her own marriage.    Jur...
  • University of Dar es Salaam among top 100 Universities in Africa
    The university of Dar-es-Salaam has ranked fourth among top 100 popular universities and higher learning institutions in Africa. This is acc...
  • Admission of Diploma holders into Higher
    TANZANIA COMMISSION FOR UNIVERSITIES Admission of Diploma holders into Higher Education Institutions for the academic year 2013/2014. The T...
  • Community Relations Manager – (One Post)
    Community Relations Manager – (One Post) African Barrick Gold (ABG) Date Listed: May 15, 2013 Email Address: ...
  • Kim Kardashian awateka tena mashabiki kwa mavazi
    Kim Kardashian aliweza tena kuuteka umati waliohudhuria katika sherehe za kuchangisha fedha kwa ajili ya mfuko wa kuchangisha fedha kwa ajil...

Categories

  • Africa (1)
  • Announcement (13)
  • Biashara (17)
  • Breaking News (4)
  • Burudani (11)
  • East Africa News (19)
  • Education (12)
  • Entertainment (8)
  • Fashions (1)
  • Habari (41)
  • Health (1)
  • International News (14)
  • Jamii (11)
  • Jobs (120)
  • Latest Sports News (3)
  • Local News (59)
  • Makala (8)
  • Michezo (25)
  • Music (5)
  • News (12)
  • Scholarships (4)
  • Scholarships- Jobs (7)
  • Siasa (1)
  • Sport (64)
  • sports (18)
  • Technology (2)
  • Tetesi za Usajili (9)
  • usajili (1)

Blog Archive

  • ▼  2013 (335)
    • ►  September (9)
    • ►  August (18)
    • ▼  July (23)
      • Orodha ya TBS ya bidhaa 48 zisizotakiwa kuonekana ...
      • Madawa ya Kulevya Tanzania!
      • Kitchee FC vs. Manchester United 2:5 All Goals & H...
      • Fast-changing nature of world trade poses new poli...
      • Entrepreneurship skills vital in primary schools s...
      • EADB Receives EUR25 Million for SME Financing
      • MANCHESTER YAZIDI KUFANYA VIBAYA BAADA YAICHAPWA 3...
      • The East African Round Up
      • Mission Logistics Officer/ Receptionist
      • African Barrick Gold continues to support communit...
      • Smile for Tanzania education
      • SCHOLARSHIPS FOR TANZANIAN WOMEN
      • Chadema yaitesa CCM uchaguzi wa udiwani Arusha
      • Waliokamatwa na `unga`wa mabilioni ni mabinti
      • Neymar scores 45 yard goal in Lionel Messi charity...
      • Tofauti KUBWA kati ya Marekani na Tanzania.
      • Mabilionea Tanzania wakutana na Obama
      • 2013 Linux Foundation Linux Training Scholarship P...
      • ICT and Pedagogical Development 2013 C
      • Violent Episodes Grow in Tanzania, an African Haven
      • VIDEO: Obama dancing along to Tanzania’s brass dan...
      • Obama in Tanzania, sees Africa as next global econ...
      • Obama in Tanzania, sees Africa as next global econ...
    • ►  June (27)
    • ►  May (91)
    • ►  April (53)
    • ►  March (41)
    • ►  February (59)
    • ►  January (14)
  • ►  2012 (162)
    • ►  December (42)
    • ►  November (70)
    • ►  October (50)
Powered by Blogger.

About Me

Unknown
View my complete profile