MAKANGALESOPHIE

  • Subscribe to our RSS feed.
  • Twitter
  • StumbleUpon
  • Reddit
  • Facebook
  • Digg

Saturday, 24 November 2012

Mawaziri wazomewa mbele ya Kinana

Posted on 00:09 by Unknown
MAWAZIRI watatu wa Rais Jakaya Kikwete juzi walizomewa baada ya kupanda jukwaani kujibu kero mbalimbali za wananchi katika mkutano wa kwanza wa viongozi wapya wa CCM taifa, ulioongozwa na Katibu Mkuu wake, Abdulrahaman Kinana.

Tukio hilo lilitokea juzi mkoani Mtwara ambako Kinana na mawaziri hao walikuwa katika ziara ya chama kujibu kero mbalimbali za wananchi.Mawaziri waliokumbwa na dhahama hiyo ni Christopher Chiza wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Hawa Ghasia (Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa - Tamisemi) Naibu wake, Aggrey Mwanri.

Chiza ndio alikuwa wa kwanza kukumbana na zomeazomea hiyo, lakini mambo yalikuwa magumu zaidi kwa Ghasia ambaye alizomewa tangu alipoanza kuzungumza mpaka alipomaliza.Ghasia ambaye pia ni mbunge wa Mtwara Vijijini, alirushiwa makombora na Rukia Ismail Athumani ambaye alimshutumu yeye pamoja na Mbunge wa Mtwara mjini, Asnein Murji kwamba waliruhusu gesi kupelekwa Dar es Salaam wakati wananchi wa mkoa huo hawajafaidika nayo.

“Ghasia na Murji kwanini mnaudanganya umma kwa kupeleka gesi Dar es Salaam, sisi hatuna ubaya na chama ila hatutaki gesi iende huko” alisema Athumani huku akishangiliwa na mamia ya watu waliohudhuria mkutano huo.Kabla ya dada huyo kuteka hisia za wananchi kwa kuwasilisha kero hiyo, Kinana alimruhusu mwananchi mwingine, Issa Kambona ambaye pia alieleza kuwa hakubaliani na suala la gesi hiyo kupelekwa Dar es Salaam.

Kinana alisema amesikia hoja hizo za wananchi na kwamba atamueleza Waziri wa Nishati na Madini azungumze na wananchi wa Mtwara kuhusu gesi hiyo.Baada ya mambo kuzidi kuwa magumu, Ghasia alilazimika kupanda jukwaani kujibu makombora aliyokuwa akirushiwa na wananchi waliofika katika mkutano huo.

“Sio kweli kwamba hatutetei maslahi yenu, gesi iliyopo ni nyingi hamuwezi kuitumia na kuimaliza, kuna futi za ujazo trilioni 20,000 na tunaweza kuitumia kwa zaidi ya miaka 90, hata hivyo, Wizara ya Nishati na Madini imetoa ofa ya kuwalipia chuo vijana 150 kila mwaka,” alisema Ghasia, lakini wananchi hao waliendelea kumzomea.“Uongo, uongo, hatutaki, hatutaki, huyoo, huyooo” walisikika wakisema wananchi hao, hali iliyomfanya Katibu wa Itikadi na Uenezi wa chama hicho, Nape Nnauye kuingilia kati, kujaribu kuwatuliza.

“Kelele unazozisikia dada (Ghasia) zinaashiria kuna jambo, nafasi hizo 150 hawazipati, kama zinatolewa basi kwa upendeleo,” alisema Nape huku akishangiliwa na wananchi hao.Baada ya hali kutulia kiasi, Ghasia alijaribu kuendelea kutoa ufafanuzi, lakini kitendo cha kuanza kuzungumza, wananchi hao walianza tena kuzomea.

“Kila mtu amelelewa katika mazingira tofauti, hilo halinihusu…watu wangu wa Mtwara vijijini wamenielewa,” alisema Ghasia na kuteremka jukwaani hali iliyozidisha kelele za kumzomea.Nape alisawazisha mambo kwa kusema, hoja ya wananchi hao imechukuliwa na itawasilishwa kwa Serikali ili kuona namna ambavyo inaweza kukaa na wananchi hao na kuweka maslahi yao mbele.

Ilivyoanza
Panzia la zomea zomea lilifunguliwa na Chiza alipopanda jukwaani kujibu hoja ya kuyumba kwa soko la zao la korosho, ambapo wananchi walimpinga baadhi ya kauli alizozitoa.“Tatizo la korosho ni baadhi ya viongozi wa vyama vya ushirika na wengine ni watendaji wa Serikali …nipo hapa na wala siondoki, nitalishughulikia hili ili korosho zinunuliwe” alisema Chiza huku sauti za wananchi zikimpinga kwa kusema “uongooo”.

Hata hivyo, Chiza aliweza kukabiliana na hali ya zomeazomea jukwaani baada ya watuliza wananchi kwa kusisitiza kuwa ataendelea kuwapo Mtwara, kushughulikia tatizo hilo ili ununuzi uendelee.Naibu Waziri wa Tamisemi, Mwanri alipata wakati mgumu mara alipopanda jukwaani na kuanza kuzungumzia namna ya kumaliza kero ndogondogo zinazoletwa na mamlaka zake, wananchi walikuwa wanazoea “huyoo…hatutaki” lakini baada ya kuanza kuongea alionekana kuiteka hadhira na mambo yakawa shwari. “

“Tumesema wauza vitumbua, wasibughudhiwe … mkurugenzi njoo jukwani, nakuagiza kuanzia leo marufuku wanafunzi kurudishwa shuleni kwa sababu ya michango” alisema Mwanri huku akishangiliwa.Awali Kinana alisema mkutano huo unalenga kuzipatia ufumbuzi kero za wananchi ambazo zinawezakuwa kikwazo kwa chama hicho kuingia madarakani mwaka 2015.

Katibu mkuu huyo wa chama tawala alisema umefika wakati wa chama kusimamia utendaji wa Serikali kutatua kero za wananchi wa mkoa wa Mtwara ikiwa ni pamoja na kuyumba kwa soko la korosho na gesi.“Najua hapa kuna kero kubwa mbili, korosho na gesi, nimekuja na Mawaziri hapa watatoa majibu leo” alisema Kinana huku akishangiliwa na umati mkubwa wa watu ulioudhuria mkutano huo.

Sifa mgombea urais
Katika hatua nyingine, Kinana amevunja ukimya kuhusu mbio za urais mwaka 2015 na kusema CCM itamtosa bila kumuonea haya mwanachama yeyote atakayeomba kuteuuliwa kugombea urais kwa tiketi yake, huku akiwa kinara wa kutegemea makundi kumwigiza katika nafasi hiyo.Badala yake akaeleza kuwa chama hicho kitamteua mgombea mwadilifu, anayekubalika na watu na asiye na makundi.

Mbali na sifa hizo Kinana pia ameeleza kuwa mgombea huyo wa CCM atakuwa msafi, makini, mchapakazi, mzalendo ambaye anajali maslahi ya wananchi na kwamba Mei 2015 wataanza kutoa fomu kwa wana CCM wanaowania nafasi hiyo.Kinana alisema hayo jana katika kijiji cha Isesa, Sumbawanga Mjini wakati akifungua tawi la CCM na kuzungumza na wanachama.

Katika kipindi cha kuuliza maswali, wanachama hao walitaka kufahamu namna chama hicho kilichojipanga kumpata mgombea urais makini ambaye hatakuwa mzigo kumnadi dhidi ya wapinzani.“Tumejipanga vizuri, atapatikana mgombea urais bora, vigezo vipo wazi tunataka mgombea urais mwadilifu, makini, mchapakazi, mzalendo ambaye anakubalika na wananchi,”alisema Kinana.

Aliongeza kwamba chama hicho kitatoa fomu kwa wanaotaka kuwania nafasi hiyo na vikao vya chama ndivyo vitakavyoamua,”alisema Kinana.“Tuna utaratibu mzuri wa kupata wagombea urais bora kwa sababu vigezo vyote viko wazi na kwamba wagombea hao watapimwa kwa vigezo hivyo,” alisema Kinana.

Alisema Wanasumbawanga wasiwe na wasiwasi watampata mgombea ambaye atakuwa mwiba kwa vyama vya upinzani.Alisema kiongozi mwenye makundi na asiyekuwa mwadilifu hatakuwa na nafasi ya kuteuliwa na chama hicho kugombea urais.“Haya si maneno yangu bali ni vigezo vya chama vilivyo wazi ambavyo vinatumiwa kwa kila mgombea wa nafasi hiyo kubwa kushinda zote,” alisema

Alisema anakifahamu chama hicho na kwamba kitavitumia vigezo hivyo ili kupata mgombea urais ambaye wananchi wanamkubali.Awali wanachama wa chama hicho wakiongea kwa hisia kali, walisema wanataka chama hicho kimsimamishe mgombea urais atakayekuwa mwiba kwa wapinzani.

“Tunayasikia majina ya watu wanaowania nafasi hizo, chonde chonde katibu mkuu tunaomba apatikane kiongozi ambaye hatatupatia kazi ya kumnadi, awe mwadilifu ambaye akitangazwa watu wafurahi bila kunung’unika,” alisema Peter Lilata.Alisema, “tukikosea kuteua kiongozi bora tutakuja kujuta hapo baadaye.”

Vijana CCM, Chadema nusura wazipige
Katika ufunguzi wa tawi la CCM la Isesa nusura vijana CCM na wa Chadema watwangane makonde baada ya vijana wa Chadema kuwatuhumu CCM kwamba wamewaibia bendera ya chama chao.

Mabishano kuhusu bendera hiyo yaliendelea katika kipindi chote ambacho Kinana alikuwa akizungumza na wanachama wa tawi hilo.“Hawa CCM wameng’oa bendera yetu hapa huo siyo ustaraabu ni lazima mturudishie bendera yetu vinginevyo patakuwa hapatoshi,” mmoja wa vijana wa Chadema alisikika akisema.
Hata hivyo, busara za askari polisi waliokuwa katika mkutano huo zilisaidia kuzima hasira zavijana wa Chadema.

Chanzo Gazeti la Mwananchi
Email ThisBlogThis!Share to XShare to FacebookShare to Pinterest
Posted in News | No comments
Newer Post Older Post Home
View mobile version

0 comments:

Post a Comment

Subscribe to: Post Comments (Atom)

Popular Posts

  • Christiano Ronaldo and His 29 girlfriends List.
    Chr is tiano Ronaldo is famous as a great and cool football player. He play for England Manchester United Club, at age of 26 and he already...
  • Maadhimisho ya miaka 100 ya kituo cha makumbusho ya utamaduni wa Kisukuma - BUJORA Mwanza.
    Maadhimisho ya miaka 100 ya kituo cha makumbusho ya utamaduni wa Kisukuma - BUJORA Mwanza.                 Makumbusho ya  ka...
  • Tumehuzunika kidogo, Cesc Fabregas
  • Computer System Analyst Grade I (Business Analysis) – One Post - (Re-advertised) E-Government Agency (EGA
    Computer System Analyst Grade I (Business Analysis) – One Post - (Re-advertised) E-Government Agency (EGA) Date Listed: J...
  • Post: Part-time journalist
    Post: Part-time journalist Job Description Timely and accurately collecting African real-time news and then integrate the manuscript ...
  • Tempetation
    An Ivy League-educated marriage counselor who gives marital advice but finds it difficult to address issues with her own marriage.    Jur...
  • University of Dar es Salaam among top 100 Universities in Africa
    The university of Dar-es-Salaam has ranked fourth among top 100 popular universities and higher learning institutions in Africa. This is acc...
  • Admission of Diploma holders into Higher
    TANZANIA COMMISSION FOR UNIVERSITIES Admission of Diploma holders into Higher Education Institutions for the academic year 2013/2014. The T...
  • Community Relations Manager – (One Post)
    Community Relations Manager – (One Post) African Barrick Gold (ABG) Date Listed: May 15, 2013 Email Address: ...
  • Kim Kardashian awateka tena mashabiki kwa mavazi
    Kim Kardashian aliweza tena kuuteka umati waliohudhuria katika sherehe za kuchangisha fedha kwa ajili ya mfuko wa kuchangisha fedha kwa ajil...

Categories

  • Africa (1)
  • Announcement (13)
  • Biashara (17)
  • Breaking News (4)
  • Burudani (11)
  • East Africa News (19)
  • Education (12)
  • Entertainment (8)
  • Fashions (1)
  • Habari (41)
  • Health (1)
  • International News (14)
  • Jamii (11)
  • Jobs (120)
  • Latest Sports News (3)
  • Local News (59)
  • Makala (8)
  • Michezo (25)
  • Music (5)
  • News (12)
  • Scholarships (4)
  • Scholarships- Jobs (7)
  • Siasa (1)
  • Sport (64)
  • sports (18)
  • Technology (2)
  • Tetesi za Usajili (9)
  • usajili (1)

Blog Archive

  • ►  2013 (335)
    • ►  September (9)
    • ►  August (18)
    • ►  July (23)
    • ►  June (27)
    • ►  May (91)
    • ►  April (53)
    • ►  March (41)
    • ►  February (59)
    • ►  January (14)
  • ▼  2012 (162)
    • ►  December (42)
    • ▼  November (70)
      • Defoe: The sky is the limit now I'm Jermain man.
      • Message by the Director-General International Labo...
      • IBDP Coordinator
      • PYP Coordinator
      • Jinsi tunavyojenga msingi wa kuwachukia wenzetu***
      • CRDB limited has recorded an impressive financial ...
      • PRESS RELEASE
      • Fastjet unveiled its first fully branded aircraft.
      • Project Leader - Serengeti National Park, Tanzania
      • Overseas Research Fellow/ Lecturer (Tanzania)
      • Ratiba ya mikutano ya Maoni ya Katiba Halimashauri...
      • Chadema uongozi balaa
      • Mawaziri wazomewa mbele ya Kinana
      • Governments and businesses must give local people ...
      • East African Round Up News
      • Another big land clashes is escalating between the...
      • “ICT STAR
      • Urgent Opening for SBU Head (paints) at East Afric...
      • Aga Khan University, East Africa
      • Resident Engineer - Bus Rapid Transit System - Tan...
      • Roman Abramovich amtimua rasmi Roberto Di Mateo
      • Sir Alex Ferguson's hands shaking !! The most pain...
      • Gari la Tevez lasombwa na Karandinga
      • President Kagame opens Gorillas Golf Hotel in Nyar...
      • Simba sack members, committees
      • (Sida) and (AGRA) announced a USD10 million grant ...
      • Mchukueni Theo na £8m nipatieni Raheem Sterling,...
      • UGANDA: Police declare war on cattle rustlers
      • Badilika Mancini amwambia Balotelli
      • Training on process of dispute mediation, arbitrat...
      • Reduce green house gases emissions from deforestat...
      • INTERVIEW WITH THE HUAWEI MANAGING DIRECTOR MR. BR...
      • HUAWEI LAUNCHES “ICT STAR” PROGRAM FOR TANZANIA ED...
      • Bi Kidude: aendelea kuishi…
      • THE ADVANCE OF SAMSUNG
      • Rais wa Uruguay Jose Mujica ndie rais masikini zai...
      • Manchester United Vs Aston Villa 3-2 all goals Eng...
      • Research Fellow / Project Manager
      • Tax Manager - Big 4 Tanzania
      • Sudanese journalist found after being abducted, to...
      • Fashion That Makes Us Sad: Jean-Flops
      • Manchester United & Arsenal make Forbes top ten
      • Liverpool ready to snatch £4m Manchester United ta...
      • Public Health Specialist (Laboratory Advisor)-Vacancy
      • Assistant Sales officer-Vacancy
      • Receptionist / Secretary-Vacancy
      • Financial Analyst Officer
      • Financial Systems and Audit Advisor-Vacancy
      • Sheikh Mukadam aunganishwa kwenye kesi ya Sheikh P...
      • Obama has left his house and is on the way to the ...
      • President Barack Obama wins re-election
      • Taarifa ya Waziri wa Elimu kwa umma kuhusu mtihani...
      • Nataka kuwa balozi nchini Uingereza, Kim Kardashian
      • Wiki ya SAre katika picha_Ligi kuu ya Uingereza
      • Marefa wakasirika na watishia kugomea kuchezesha m...
      • Vacancy-Senior Cabin Crew
      • Young Leaders Project Coordinator
      • Assistant Accountant Officer
      • Research Manager
      • Journalism Trainer/Mentor
      • Project Manager, Resilience
      • Programme Assistant, Resilience
      • Administrative Assistant
      • Administrative Assistant/Logistics
      • Programme Officer: Documentary and Future
      • Administrative assistant
      • Programme Officer: Culture and Governance
      • Director of Finance and Administration
      • Tanzania stands a chance to be an HIV-free generat...
      • UNICEF has commended the continued contribution of...
    • ►  October (50)
Powered by Blogger.

About Me

Unknown
View my complete profile