MAKANGALESOPHIE

  • Subscribe to our RSS feed.
  • Twitter
  • StumbleUpon
  • Reddit
  • Facebook
  • Digg

Monday, 12 November 2012

Rais wa Uruguay Jose Mujica ndie rais masikini zaidi duniani kwa sasa!

Posted on 06:10 by Unknown
NCHI ya Uruguay yenye raia takribani milioni 4, inatajwa kuwa na bahati ya kuwa na Rais asiye na chembe ya tamaa. Hana makuu, kiasi
kwamba anatajwa kuwa ndiye Rais masikini zaidi kuwahi kutokea duniani.

Huyu si mwingine, bali ni Jose Mujica, Rais wa sasa wa Uruguay ambaye pia ni Rais wa 40 wa nchi hiyo. Tangu aingie madarakani Machi mosi
mwaka 2010, amekuwa akionekana kuwa kiongozi wa tofauti kabisa, tofauti na waliomtangulia. 
Raisi wa Uruguay, Jose Mujica
 
 
 Mathalan, baada ya kufanikiwa kuishika nchini, hakuwa na tamaa ya kukimbilia Ikulu, yeye alichokifanya ni kuamua kuishi katika makazi
yake yaleyale, katika nyumba ya mkewe iliyoko shambani, nje ya Jiji la Montevideo.

Kwa ujumla, anapenda maisha ya kawaida, maisha ya kuwahurumia wengine na kujitahidi kuonesha kwa vitendo.

Ni vigumu kuamini, licha ya kuwa ni Rais wa nchi, amejishusha mno kiasi cha mara kadhaa kuonekana akijichanganya na raia wake katika
shughuli za ujenzi wa taifa, ikiwamo ujenzi wa barabara, kulima mashamba ya mfano.

Na wakati mwingine, anapougua huwahi kupanga mstari ili kuonana na daktari, akichelewa anapanga mstari kusubiri zamu yake.

Ni Rais pekee ambaye ameamua kutoa mshahara wake kwa zaidi ya asilima 90 kugawana na watu masikini wa nchi yake, kwamba fedha hizo huingizwa
katika vikundi mbalimbali vya maendeleo.

Akiwa amepangiwa na Bunge kupokea dola za Kimarekani 11,000 (sh milioni 17.6 kwa fedha za Tanzania) kwa mwezi, hajawahi kupokea fedha
hizo na ameiamuru Hazina kuzipeleka fedha hizo kwa wananchi masikini.

Yeye hupokea shilingi milioni 3 tu, tena hizi akizitumia kwa ajili ya mafuta ya gari lake alilonunua na mkewe aina ya Volkswagon Beetle
maarufu kama `Mgongo wa Chura’. Gari hilo lenye umri wa miaka 23, ndio utajiri pekee anaojivunia. 
 
 
Mkoko ndani ya Gereji ya Raisi Jose Mujica
 
 
Hana kingine anachokimiliki. Hana akaunti benki, hana nyumba yake binafsi, wala mali nyingine ya aina yoyote aliyojilimbikizia.
Kuhusiana na gari lake lenye thamani ya dola za Kimarekani 1,900 (Sh milioni 3), ambalo analiendesha mwenyewe, anasema:

“Niko mimi na mke wangu, wawili tu, gari kubwa la nini, sina haja nalo, sitaki kuwaibia wananchi, kunichagua tu kuwaongoza ni sifa
pekee, tena kubwa inayokaribia utukufu wa kawaida, sasa zaidi ya hapo nini…

“Nahitaji sana kuwatumikia wananchi wa Uruguay, sio kuwanyonya wala kuwaibia au kuwa mwanya wa kuchuma na kujifurahisha mimi, mke wangu,
watoto wangu na ndugu zangu, sioni haja hiyo na sitaki kuwa mnyonyaji kamwe,” anasema Rais Mujica. Anasisitiza anayafurahia maisha ya
kawaida, hivyo haoni shida kuishi na watu wa kawaida mtaani kwake, kupiga nao porojo na hata kushirikiana katika shughuli za kijamii pale
inapolazimu.

“Nikiwa na akaunti benki, nikiwa na magari makubwa, nitakuwa nakaribisha ushawishi wa kuwa mwizi, kuwaibia wananchi wangu, sitaki
chochote,” anaongeza Rais huyo ambaye hata anapoamua kunyoa nywele zake, hahitaji kinyozi maalumu, bali yeyote anayejua kunyoa anamwita
nyumbani kwake aweze kumnyoa.

Staili ya maisha ya Rais huyo inaonekana pia kumwingia mkewe ambaye pia tofauti na wake wengine wa marais, yeye hajipambi kwa dhahabu,
almasi wala aina nyingine ya vito vya thamani.

Anashirikiana na mumewe katika shamba lao la maua katika makazi yao, huku Rais Mujica wakati mwingine akifanya usafi wa nyumba na hata
kumwagilia maua. Hayo ndiyo maisha ya Jose Mujica, Rais wa 40 wa Uruguay ambaye kwa sasa ana umri wa miaka 77, lakini licha ya
kupigania mno kuingia Ikulu, ameonesha kutokuwa na kiu ya utajiri, hataki kujikweza na wala kuonekana ni tofauti na watu wengine.

Ndiyo maana ameonekana kuwa Rais wa ajabu, akitajwa pengine kuwa ndiye asiye na makuu na masikini kuliko wote duniani. Hata vaa yake ni ya
kawaida, mara nyingi akiingia ofisini na mavazi ya kawaida, lakini mara moja moja tu, akivalia suti na tai hasa anapokuwa na ugeni mzito.

Angalau Makamu wake, Danilo Astori anaonekana na `ufisadi’ kidogo, kwani ana nyumba yenye thamani ya dola 250,000 (Sh milioni 400) na
gari kama la milioni 30 hivi. Je, kuna wengine wenye staili ya maisha ya Rais Mujica? Yawezekana, lakini kwa sasa imeonekana hakuna kama
Mujica.

Rais Mujica akiteremka ndani ya mkoko wake































































Email ThisBlogThis!Share to XShare to FacebookShare to Pinterest
Posted in International News | No comments
Newer Post Older Post Home
View mobile version

0 comments:

Post a Comment

Subscribe to: Post Comments (Atom)

Popular Posts

  • Christiano Ronaldo and His 29 girlfriends List.
    Chr is tiano Ronaldo is famous as a great and cool football player. He play for England Manchester United Club, at age of 26 and he already...
  • Maadhimisho ya miaka 100 ya kituo cha makumbusho ya utamaduni wa Kisukuma - BUJORA Mwanza.
    Maadhimisho ya miaka 100 ya kituo cha makumbusho ya utamaduni wa Kisukuma - BUJORA Mwanza.                 Makumbusho ya  ka...
  • Tumehuzunika kidogo, Cesc Fabregas
  • Computer System Analyst Grade I (Business Analysis) – One Post - (Re-advertised) E-Government Agency (EGA
    Computer System Analyst Grade I (Business Analysis) – One Post - (Re-advertised) E-Government Agency (EGA) Date Listed: J...
  • Post: Part-time journalist
    Post: Part-time journalist Job Description Timely and accurately collecting African real-time news and then integrate the manuscript ...
  • Tempetation
    An Ivy League-educated marriage counselor who gives marital advice but finds it difficult to address issues with her own marriage.    Jur...
  • University of Dar es Salaam among top 100 Universities in Africa
    The university of Dar-es-Salaam has ranked fourth among top 100 popular universities and higher learning institutions in Africa. This is acc...
  • Admission of Diploma holders into Higher
    TANZANIA COMMISSION FOR UNIVERSITIES Admission of Diploma holders into Higher Education Institutions for the academic year 2013/2014. The T...
  • Community Relations Manager – (One Post)
    Community Relations Manager – (One Post) African Barrick Gold (ABG) Date Listed: May 15, 2013 Email Address: ...
  • Kim Kardashian awateka tena mashabiki kwa mavazi
    Kim Kardashian aliweza tena kuuteka umati waliohudhuria katika sherehe za kuchangisha fedha kwa ajili ya mfuko wa kuchangisha fedha kwa ajil...

Categories

  • Africa (1)
  • Announcement (13)
  • Biashara (17)
  • Breaking News (4)
  • Burudani (11)
  • East Africa News (19)
  • Education (12)
  • Entertainment (8)
  • Fashions (1)
  • Habari (41)
  • Health (1)
  • International News (14)
  • Jamii (11)
  • Jobs (120)
  • Latest Sports News (3)
  • Local News (59)
  • Makala (8)
  • Michezo (25)
  • Music (5)
  • News (12)
  • Scholarships (4)
  • Scholarships- Jobs (7)
  • Siasa (1)
  • Sport (64)
  • sports (18)
  • Technology (2)
  • Tetesi za Usajili (9)
  • usajili (1)

Blog Archive

  • ►  2013 (335)
    • ►  September (9)
    • ►  August (18)
    • ►  July (23)
    • ►  June (27)
    • ►  May (91)
    • ►  April (53)
    • ►  March (41)
    • ►  February (59)
    • ►  January (14)
  • ▼  2012 (162)
    • ►  December (42)
    • ▼  November (70)
      • Defoe: The sky is the limit now I'm Jermain man.
      • Message by the Director-General International Labo...
      • IBDP Coordinator
      • PYP Coordinator
      • Jinsi tunavyojenga msingi wa kuwachukia wenzetu***
      • CRDB limited has recorded an impressive financial ...
      • PRESS RELEASE
      • Fastjet unveiled its first fully branded aircraft.
      • Project Leader - Serengeti National Park, Tanzania
      • Overseas Research Fellow/ Lecturer (Tanzania)
      • Ratiba ya mikutano ya Maoni ya Katiba Halimashauri...
      • Chadema uongozi balaa
      • Mawaziri wazomewa mbele ya Kinana
      • Governments and businesses must give local people ...
      • East African Round Up News
      • Another big land clashes is escalating between the...
      • “ICT STAR
      • Urgent Opening for SBU Head (paints) at East Afric...
      • Aga Khan University, East Africa
      • Resident Engineer - Bus Rapid Transit System - Tan...
      • Roman Abramovich amtimua rasmi Roberto Di Mateo
      • Sir Alex Ferguson's hands shaking !! The most pain...
      • Gari la Tevez lasombwa na Karandinga
      • President Kagame opens Gorillas Golf Hotel in Nyar...
      • Simba sack members, committees
      • (Sida) and (AGRA) announced a USD10 million grant ...
      • Mchukueni Theo na £8m nipatieni Raheem Sterling,...
      • UGANDA: Police declare war on cattle rustlers
      • Badilika Mancini amwambia Balotelli
      • Training on process of dispute mediation, arbitrat...
      • Reduce green house gases emissions from deforestat...
      • INTERVIEW WITH THE HUAWEI MANAGING DIRECTOR MR. BR...
      • HUAWEI LAUNCHES “ICT STAR” PROGRAM FOR TANZANIA ED...
      • Bi Kidude: aendelea kuishi…
      • THE ADVANCE OF SAMSUNG
      • Rais wa Uruguay Jose Mujica ndie rais masikini zai...
      • Manchester United Vs Aston Villa 3-2 all goals Eng...
      • Research Fellow / Project Manager
      • Tax Manager - Big 4 Tanzania
      • Sudanese journalist found after being abducted, to...
      • Fashion That Makes Us Sad: Jean-Flops
      • Manchester United & Arsenal make Forbes top ten
      • Liverpool ready to snatch £4m Manchester United ta...
      • Public Health Specialist (Laboratory Advisor)-Vacancy
      • Assistant Sales officer-Vacancy
      • Receptionist / Secretary-Vacancy
      • Financial Analyst Officer
      • Financial Systems and Audit Advisor-Vacancy
      • Sheikh Mukadam aunganishwa kwenye kesi ya Sheikh P...
      • Obama has left his house and is on the way to the ...
      • President Barack Obama wins re-election
      • Taarifa ya Waziri wa Elimu kwa umma kuhusu mtihani...
      • Nataka kuwa balozi nchini Uingereza, Kim Kardashian
      • Wiki ya SAre katika picha_Ligi kuu ya Uingereza
      • Marefa wakasirika na watishia kugomea kuchezesha m...
      • Vacancy-Senior Cabin Crew
      • Young Leaders Project Coordinator
      • Assistant Accountant Officer
      • Research Manager
      • Journalism Trainer/Mentor
      • Project Manager, Resilience
      • Programme Assistant, Resilience
      • Administrative Assistant
      • Administrative Assistant/Logistics
      • Programme Officer: Documentary and Future
      • Administrative assistant
      • Programme Officer: Culture and Governance
      • Director of Finance and Administration
      • Tanzania stands a chance to be an HIV-free generat...
      • UNICEF has commended the continued contribution of...
    • ►  October (50)
Powered by Blogger.

About Me

Unknown
View my complete profile