MAKANGALESOPHIE

  • Subscribe to our RSS feed.
  • Twitter
  • StumbleUpon
  • Reddit
  • Facebook
  • Digg

Thursday, 22 August 2013

Benki ya Taifa Biashara yazindua kampeni ya kuweka akiba mashuleni

Posted on 02:45 by Unknown


Benki ya Taifa ya Biashara (NBC) imezindua kampeni ya kutoa elimu mashuleni ya usimamizi na utawala wa fedha kwa vijana katika jitihada zake za kuwaelimisha wanafunzi wa Sekondari nchi nzima umuhimu wa kuwa na utamaduni wa kuweka akiba.
Akizungumza katika uzinduzi rasmi wa kampeni hiyo jijini Dar es Salaam jana, Mkurugenzi Mtendaji wa Benki hiyo, Bi Mizinga Melu alipotembelea shule ya Sekondari ya Benjamini Mkapa ya jijini alisema kampeni ya kujifunza utamaduni wa kujiwekea akiba ni mkakati wa benki wa kuelimisha vijana mashuleni na jamii kwa jumla nchi nzima umuhimu wa kuweka akiba kwa ajili ya baadaye.
Alisema Benki ya Taifa ya Biashara inafahamu kwa kina umuhimu wa kuwekeza na kuelimisha vijana wa leo wa kitanzania jinsi ya kusimamia mapato yao na kujiwekea akiba kwa maisha yao  baadaye ili kuhakikisha wanajifunza mbinu wakiwa bado vijana wadogo mashuleni.
Melu alisisitiza kwamba vijana ndio nguzo pekee kwa maendeleo ya nchi ya kijamii, kisiasa na kiuchumi kwahiyo inahitajika juhudi za makusudi za kumpatia kijana wa leo taarifa, elimu ya fedha na ujasirimali katika mitaala ya masomo yao kwa manufaa ya nchi nzima.
Alisema kwamba kuna mambo ya muhimu kwenye stadi za maisha hasa katika swala la kujiwekea akiba kwa ajili ya baadaye kwa hiyo wanafunzi watafundishwa mbinu sahihi za kutunza fedha na mapato ili kupunguza utegemezi kwa walevi na wazazi na jamii kwa ujumla.
Melu alifafanua kwamba kampeni hii ya kufundisha utawala wa fedha na mapato kwa vijana itatengeneza mazingira mazuri kwa wanafunzi, walimu, wafanyakazi wa benki ya NBC and jamii kwa ujumla kushirikiana kwa karibu zaidi.
“Sisi NBC tunatambua umuhimu na nafasi vijana katika kutengeneza jamii ya baadaye kwa mantiki hiyo kwa kutambua uwepo wao tunajisikia ulazima wa kuwajengea uwezo kwa maslahi ya kizazi kijacho,’
Kwa upande wake Mkurugenzi wa Maendeleo ya Vijana kutoka Wizara ya Habari, Utamaduni, Maendeelo ya Vijana na Michezo ambaye alisoma hotuba ya Waziri wa Habari kwa niaba yake, Profesa Elisante Ole Gabriel alisema serikali itaendelea kutilia mkazo umuhimu wa elimu kwa vijana katika kusukuma mbele gurudumu la maendeleo ya taifa.
“Nachukua nafasi hii kuwashukuru Benki ya Taifa ya Biashara (NBC) kwa kuendesha kampeni hii, kwani tunaamini kuwa kampeni hii itawafikia vijana wengi, watakaobadili mwelekeo wao wa kujitegemea na hatimaye kujijengea uwezo wa kujitegemea kiuchumi, sasa na baadaye,” alisema 
 Profesa Gabriel aliendelea kuishukuru benki hiyo kwa kuwa mstari wa mbele katika kusaidia sekta ya elimu hapa nchini pamoja na hivi karibuni kuchangia bweni huko Tabora na Maktaba ya kujisomea huko Lindi ambayo ni moja ya changamoto kubwa sana kwa nchi na Serikali.
Serikali kupitia mwaka wa fedha 2013 na 2014 Wizara ya Habari, Utamaduni, Maendeleo ya Vijana na Michezo ilitenga kiasi cha Tsh 6.1 billioni kwa ajili ya kutoa mikopo kwa vijana nchini.
Kwa Upande wake Mkuuwa Idara ya Masoko, Mawasiliano na Mahusiano Mwinda Kiula Mfugale alisema kupitia programu ya kujitolea kwa jamii kampeni ya kuhamasisha elimu ya utawala wa fedha na kuweka akiba imefundisha wanafunzi 3,000 na malengo kufikia wanafunzi 6,000 nchi nzima.
Mwisho..
Email ThisBlogThis!Share to XShare to FacebookShare to Pinterest
Posted in Biashara | No comments
Newer Post Older Post Home
View mobile version

0 comments:

Post a Comment

Subscribe to: Post Comments (Atom)

Popular Posts

  • Christiano Ronaldo and His 29 girlfriends List.
    Chr is tiano Ronaldo is famous as a great and cool football player. He play for England Manchester United Club, at age of 26 and he already...
  • Maadhimisho ya miaka 100 ya kituo cha makumbusho ya utamaduni wa Kisukuma - BUJORA Mwanza.
    Maadhimisho ya miaka 100 ya kituo cha makumbusho ya utamaduni wa Kisukuma - BUJORA Mwanza.                 Makumbusho ya  ka...
  • Tumehuzunika kidogo, Cesc Fabregas
  • Computer System Analyst Grade I (Business Analysis) – One Post - (Re-advertised) E-Government Agency (EGA
    Computer System Analyst Grade I (Business Analysis) – One Post - (Re-advertised) E-Government Agency (EGA) Date Listed: J...
  • Post: Part-time journalist
    Post: Part-time journalist Job Description Timely and accurately collecting African real-time news and then integrate the manuscript ...
  • Tempetation
    An Ivy League-educated marriage counselor who gives marital advice but finds it difficult to address issues with her own marriage.    Jur...
  • University of Dar es Salaam among top 100 Universities in Africa
    The university of Dar-es-Salaam has ranked fourth among top 100 popular universities and higher learning institutions in Africa. This is acc...
  • Admission of Diploma holders into Higher
    TANZANIA COMMISSION FOR UNIVERSITIES Admission of Diploma holders into Higher Education Institutions for the academic year 2013/2014. The T...
  • Community Relations Manager – (One Post)
    Community Relations Manager – (One Post) African Barrick Gold (ABG) Date Listed: May 15, 2013 Email Address: ...
  • Kim Kardashian awateka tena mashabiki kwa mavazi
    Kim Kardashian aliweza tena kuuteka umati waliohudhuria katika sherehe za kuchangisha fedha kwa ajili ya mfuko wa kuchangisha fedha kwa ajil...

Categories

  • Africa (1)
  • Announcement (13)
  • Biashara (17)
  • Breaking News (4)
  • Burudani (11)
  • East Africa News (19)
  • Education (12)
  • Entertainment (8)
  • Fashions (1)
  • Habari (41)
  • Health (1)
  • International News (14)
  • Jamii (11)
  • Jobs (120)
  • Latest Sports News (3)
  • Local News (59)
  • Makala (8)
  • Michezo (25)
  • Music (5)
  • News (12)
  • Scholarships (4)
  • Scholarships- Jobs (7)
  • Siasa (1)
  • Sport (64)
  • sports (18)
  • Technology (2)
  • Tetesi za Usajili (9)
  • usajili (1)

Blog Archive

  • ▼  2013 (335)
    • ►  September (9)
    • ▼  August (18)
      • USAJILI WA GARETH BALE KWENDA REAL MADRID WAIVA
      • Chelsea join race for Willian,Bale's Madrid move i...
      • Maeneo ya Dar yakosa umeme baada ya moto kuunguza ...
      • Benki ya Taifa Biashara yazindua kampeni ya kuweka...
      • Real Madrid are rumoured to be holding the number ...
      • Just like OBAMA and OPRAH , Robert Kelly will aslo...
      • Oprah tells her Serengeti trip story through photos
      • Wenger kumgeukia Michu
      • MIWANI PANA YA EDO ~ TATHMINI YA MECHI YA KWANZA Y...
      • University of Dar es Salaam among top 100 Universi...
      • Cristiano Ronaldo's future at Real Madrid remains ...
      • THIAGO ALCANTARA KULETA MZOZO BAYERN!!
      • Clinton atua Dar kiaina
      • Vichwa vya Magazeti leo kuhusu usajili Barani Ulaya
      • REAL MADRID NA MANCHESTER UNITED KWENYE MAZUNGUMZO...
      • Real Madrid stars worried Ronaldo will leave
      • Waziri Mkuu Pinda ashtakiwa mahakamani
      • Waziri Mkuu Pinda ashtakiwa mahakamani
    • ►  July (23)
    • ►  June (27)
    • ►  May (91)
    • ►  April (53)
    • ►  March (41)
    • ►  February (59)
    • ►  January (14)
  • ►  2012 (162)
    • ►  December (42)
    • ►  November (70)
    • ►  October (50)
Powered by Blogger.

About Me

Unknown
View my complete profile