MAKANGALESOPHIE

  • Subscribe to our RSS feed.
  • Twitter
  • StumbleUpon
  • Reddit
  • Facebook
  • Digg

Sunday, 4 August 2013

Clinton atua Dar kiaina

Posted on 21:39 by Unknown
Dar es Salaam. Rais wa Mstaafu wa Marekani, Bill Clinton jana alifanya ziara katika makazi ya watu duni eneo la Vingunguti, wilayani Ilala Dar es Salaam, ambapo alikagua miradi midogomidogo ya wananchi inayofadhiliwa na mfuko wake (Bill Clinton Foundation).
Rais Jakaya Kikwete akimpokea mgeni wake rais Mstaafu wa Marekani Bill Clinton anayepanda kwenye gari
Clinton alitembelea eneo hilo akitokea moja kwa moja Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere Dar es Salaam (JNIA), alipowasili akiwa katika ziara ya nchi mbalimbali za Afrika kukagua miradi inayoendeshwa na mfuko wake.
Katika eneo hilo rais huyo mstaafu alipokewa kwa shamrashamra mbalimbali ikiwamo ngoma za kiasili huku baadhi ya wananchi wakipigwa butwaa na kutoamini macho yao kwa kiongozi huyo kutembelea makazi yao.
Aidha, Clinton alipata wasaa wa kusalimiana na wakazi wa Vingunguti wakiwamo watoto ambao walishindwa kuzuia hisia zao wakijaribu kumsogelea, hali iliyomsukuma Clinton kuwasogelea na kuwasalimia kwa kuwashika mikono.
Maneno ya ‘Welcome Vingunguti Clinton‘ yalisisika kutoka kwa wananchi kuashiria kumkaribisha rais huyo wa 42 wa Marekani wakati alipowasalimia akitumia takriban dakika 15.
Clinton alikagua miradi ya midogomodogo ya wananchi iliyo chini ya mfuko wake ikiratibiwa na kutekelezwa na Shirika la Kimataifa la Kuhudumia Watoto (Plan) pamoja na Benki ya Barclays kupitia Vikoba.
Miradi aliyokagua ni pamoja na saluni za kinamama, ushonaji na chips ambapo pia alishuhudia mmoja wa wanachama wa vikundi hivyo akikabidhiwa mkopo wa Sh100,000 ambaye alieleza mbele ya Clinton kuwa atazitumia kwa mradi wa maandazi, hali iliyomfanya rais huyo na umati wa watu uliohudhuria kucheka.
Akizungumza katika ziara hiyo Clinton alizishauri benki nchini, kuwekeza kwenye vikundi vya kuweka na kukopa (Vikoba) akieleza kuwa ndiyo mkombozi kwa wananchi hasa wanawake.
“Nimekuwa kwenye miradi hii kwa miaka 30 kabla sijawa rais, hivyo basi najua umuhimu wake. Benki zinatakiwa zisaidie Vikoba kwani vikundi hivyo huwafikia wananchi kwa haraka na wepesi hivyo basi kunahitajika njia mbadala za kuhakikisha vinakuwa imara,” alisema Clinton na kuongeza;
“ Raha ya maendeleo ni kuona watu wanajitegemea wenyewe katika shughuli za kujiingizia kipato.”
Mmoja wa wananchi walionufaika, Zainab Paul ambaye ni mwanachama wa Kikundi cha Amani Hisa alisema kuwa kupitia Mfuko wa Bill Clinton na Vikoba ameweza kujikwamua kimaisha ikiwamo kumlipa mtoto wake karo ya shule.
“Kikundi chetu kina wanachama 30 na huwa tunanunua hisa kwa Sh2000 na kila mwanachama anaruhusiwa kukopa zaidi ya mara tatu,” alisema Paul.

 Clinton alieleza kufurahishwa kwake na hatua walizofikia wakazi hao wa Vingunguti akiwapongeza kinamama kwa jitihada zao na baada ya ziara hiyo alielekea Ikulu kwa mazungumzo na Rais Jakaya Kikwete.
Awali, Mtendaji Mkuu wa Plan, Tanzania, Jorgen Haldorsen alisema shirika lake limekuwa likihudumia nyanja za kiuchumi na kijamii kwa lengo la kuhakikisha wananchi wa kada ya chini wanapata huduma mbalimbali ikiwamo afya.
Naye, Mshauri wa Mambo ya Kujikimu wa Plan Stella Tungaraza aliwataka wananchi kujiunga zaidi na Vikoba na kwamba shirika lake limepanga kuanza kutoa mafunzo ujasiriamali kwa vijana ili waweze kujikwamua kiuchumi.
Baadaye Rais Clinton alitia saini makubaliano ya taasisi yake ya Bill Clinton Foundation kusaidia sekta ya kilimo nchini.
Makubaliano hayo yalitiwa saini Ikulu jijini Dar es Salaam na Sophia Kaduma ambaye ni Kaimu Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo na Chakula pamoja na mwakilishi wa taasisi ya rais huyo mstaafu, Walker Morris.
Akizungumza katika hafla hiyo, Rais Clinton alisema wakulima wa Tanzania wanatakiwa kutambua kuwa kuna nchi nyingine zinashindwa kuendesha shughuli za kilimo kutokana na uhaba wa ardhi au kuwa na ardhi isiyokuwa na rutuba na kuwataka watumie fursa hiyo kukuza uzalishaji wa kilimo .
Alisema kama wakulima hao watajituma Tanzania inaweza kuzalisha chakula ambacho kinaweza kulisha dunia.


 Chanzo cha habari na gazeti la Mwananchi.












































Email ThisBlogThis!Share to XShare to FacebookShare to Pinterest
Posted in Habari | No comments
Newer Post Older Post Home
View mobile version

0 comments:

Post a Comment

Subscribe to: Post Comments (Atom)

Popular Posts

  • Christiano Ronaldo and His 29 girlfriends List.
    Chr is tiano Ronaldo is famous as a great and cool football player. He play for England Manchester United Club, at age of 26 and he already...
  • Maadhimisho ya miaka 100 ya kituo cha makumbusho ya utamaduni wa Kisukuma - BUJORA Mwanza.
    Maadhimisho ya miaka 100 ya kituo cha makumbusho ya utamaduni wa Kisukuma - BUJORA Mwanza.                 Makumbusho ya  ka...
  • Tumehuzunika kidogo, Cesc Fabregas
  • Computer System Analyst Grade I (Business Analysis) – One Post - (Re-advertised) E-Government Agency (EGA
    Computer System Analyst Grade I (Business Analysis) – One Post - (Re-advertised) E-Government Agency (EGA) Date Listed: J...
  • Post: Part-time journalist
    Post: Part-time journalist Job Description Timely and accurately collecting African real-time news and then integrate the manuscript ...
  • Tempetation
    An Ivy League-educated marriage counselor who gives marital advice but finds it difficult to address issues with her own marriage.    Jur...
  • University of Dar es Salaam among top 100 Universities in Africa
    The university of Dar-es-Salaam has ranked fourth among top 100 popular universities and higher learning institutions in Africa. This is acc...
  • Admission of Diploma holders into Higher
    TANZANIA COMMISSION FOR UNIVERSITIES Admission of Diploma holders into Higher Education Institutions for the academic year 2013/2014. The T...
  • Community Relations Manager – (One Post)
    Community Relations Manager – (One Post) African Barrick Gold (ABG) Date Listed: May 15, 2013 Email Address: ...
  • Kim Kardashian awateka tena mashabiki kwa mavazi
    Kim Kardashian aliweza tena kuuteka umati waliohudhuria katika sherehe za kuchangisha fedha kwa ajili ya mfuko wa kuchangisha fedha kwa ajil...

Categories

  • Africa (1)
  • Announcement (13)
  • Biashara (17)
  • Breaking News (4)
  • Burudani (11)
  • East Africa News (19)
  • Education (12)
  • Entertainment (8)
  • Fashions (1)
  • Habari (41)
  • Health (1)
  • International News (14)
  • Jamii (11)
  • Jobs (120)
  • Latest Sports News (3)
  • Local News (59)
  • Makala (8)
  • Michezo (25)
  • Music (5)
  • News (12)
  • Scholarships (4)
  • Scholarships- Jobs (7)
  • Siasa (1)
  • Sport (64)
  • sports (18)
  • Technology (2)
  • Tetesi za Usajili (9)
  • usajili (1)

Blog Archive

  • ▼  2013 (335)
    • ►  September (9)
    • ▼  August (18)
      • USAJILI WA GARETH BALE KWENDA REAL MADRID WAIVA
      • Chelsea join race for Willian,Bale's Madrid move i...
      • Maeneo ya Dar yakosa umeme baada ya moto kuunguza ...
      • Benki ya Taifa Biashara yazindua kampeni ya kuweka...
      • Real Madrid are rumoured to be holding the number ...
      • Just like OBAMA and OPRAH , Robert Kelly will aslo...
      • Oprah tells her Serengeti trip story through photos
      • Wenger kumgeukia Michu
      • MIWANI PANA YA EDO ~ TATHMINI YA MECHI YA KWANZA Y...
      • University of Dar es Salaam among top 100 Universi...
      • Cristiano Ronaldo's future at Real Madrid remains ...
      • THIAGO ALCANTARA KULETA MZOZO BAYERN!!
      • Clinton atua Dar kiaina
      • Vichwa vya Magazeti leo kuhusu usajili Barani Ulaya
      • REAL MADRID NA MANCHESTER UNITED KWENYE MAZUNGUMZO...
      • Real Madrid stars worried Ronaldo will leave
      • Waziri Mkuu Pinda ashtakiwa mahakamani
      • Waziri Mkuu Pinda ashtakiwa mahakamani
    • ►  July (23)
    • ►  June (27)
    • ►  May (91)
    • ►  April (53)
    • ►  March (41)
    • ►  February (59)
    • ►  January (14)
  • ►  2012 (162)
    • ►  December (42)
    • ►  November (70)
    • ►  October (50)
Powered by Blogger.

About Me

Unknown
View my complete profile