MAKANGALESOPHIE

  • Subscribe to our RSS feed.
  • Twitter
  • StumbleUpon
  • Reddit
  • Facebook
  • Digg

Sunday, 18 August 2013

MIWANI PANA YA EDO ~ TATHMINI YA MECHI YA KWANZA YA MAN UNITED KATIKA LIGI

Posted on 00:55 by Unknown

MIWANI PANA YA EDO ~ TATHMINI YA MECHI YA KWANZA YA MAN UNITED KATIKA LIGI

nikiwa mmojawapo wa mashabiki wa mabingwa wa England Manchester United leo nimeamua kuielekeza MIWANI YANGU PANA kuangazia mechi ya kwanza katika ligi ya kocha mpya David Moyes na kilichotokea katika mchezo huo ugenini dhidi ya Swansea
RVP akifunga goli la kwanza

Najua mashabiki wengi wa United walilalamika kuona baadhi ya wachezaji wakianza katika mechi ya Jana huku wale wanaowapenda wakianzia benchi hii ni kawaida kwani mashabiki wanachojua ni ushindi tu bila kufikiria unakujaje huo ushindi.

Lakini kwa miwani yangu pana nilichogundua ni kwamba kuna baadhi ya wachezaji uwepo wao Uwanjani mara nyingi hufanya timu pinzani kuingia hofu hata kutoka kabisa kimchezo. Kuna timu zikisikia mchezaji kama  Ryan Giggs au Rio au Vidic wanaanza huingiwa na hofu na kufungwa hata kabla ya mchezo na hii hutokea katika timu nyingi na kubwa mfano Barcelona jaribu tu kuangalia ikicheza bila kuwa na mastaa wake kama Messi,Iniesta na Xavi.

Hapo ndipo utakubaliana nami kwamba uwepo wa Ryan Giggs katika kikosi kilichoanza jana ni tofauti na angeanza Januzaj au uwepo wa Valencia uwanjani ni tofauti na kama angeanza Wilfred Zaha vivyo hivyo kuanza kwa Danny Welbeck ni tofauti na angeanza Jesse Lingard au Evra ni tofauti kabisa na Buttner. Sio kama Nawadharau wachezaji hao hapana hapa nazungumzia umuhimu wa kuanza na wakongwe.
Kunaweza kukawa na potential katika vijana lakini ni vizuri kama wakianzia benchi na nadhani makocha wenye akili hulitambua hilo na hapa nampa credit David Moyes.

Turudi katika mchezo husika

Magoli Manne katika mchezo wa kwanza si haba kama tukiendelea hivi kwa mechi sita za mwanzo ambazo mimi nadhani ndizo zitakazotufanya tuwe katika nafasi ya kutetea ubingwa itakua poa sana.
Danny Welbeck anaonekana amekua kimchezo japo anahitaji kufanya mengi ili kufata nyayo za aliyekua akivaa namba 19 Dwight Yorke ila ni kati ya wachezaji watakaoisaidia United msimu huu sina shaka na hili.

Wayne Rooney bado anahitajika katika Kikosi na sioni sababu ya Kumuuza au kumruhusu aondoke hapa naziangalia dakika chache alizoingia na kutoa pasi mbili za magoli. Huyu ni aina ya wachezaji ambao United wanawahitaji msimu huu hasa kwa mchango wake katika timu na kuongeza morale katika timu.

Safu ya Ulinzi ilionekana kuimarika japokua niliona kabisa jinsi Jones alivyokua akihangaika kuziba nafasi ya Rafael na sina shaka kama alifanikiwa huku muunganiko wa Vidic na Rio Ferdinand ukionekana kua imara tuombee tu wasipate majeruhi.
Upande wa ufungaji sina shaka na Robin Van Perse kwani anajua nini anachokifanya ikifikia chance za kufunga ila hofu yangu iko katika upande wa Kiungo na mchezaji gani anayeweza kumtengenezea Van Perse pasi za magoli na hapa ndo nimeanza kumwelewa Moyes na mpango wake wa kumnunua Cesc Fabrigas kwani mipira ilikua haikai eneo hilo.

Zaidi ya yote huu ni ushindi muhimu kwa benchi zima la ufundi na timu hasa ili kuanza msimu mpya na kumsahau Ferguson kama bado yupo United.

Mechi inayofuata ni dhidi ya Chelsea Jumatatu Ijayo Nyumbani Old Trafford badae United itasafiri mpaka Liverpool kuikabili Liverpool kabla ya kurudi Old Trafford kuikaribisha Crystal Palace.

Kwa leo haya ndo niliyoyaona katika mechi hiyo na ni mawazo binafsi hayana uhusiano au hayabadilishi chochote kilichotokea.

Chanzo cha habari na blogu ya wapendasoka.blogspot.com
Email ThisBlogThis!Share to XShare to FacebookShare to Pinterest
Posted in Michezo | No comments
Newer Post Older Post Home
View mobile version

0 comments:

Post a Comment

Subscribe to: Post Comments (Atom)

Popular Posts

  • Christiano Ronaldo and His 29 girlfriends List.
    Chr is tiano Ronaldo is famous as a great and cool football player. He play for England Manchester United Club, at age of 26 and he already...
  • Maadhimisho ya miaka 100 ya kituo cha makumbusho ya utamaduni wa Kisukuma - BUJORA Mwanza.
    Maadhimisho ya miaka 100 ya kituo cha makumbusho ya utamaduni wa Kisukuma - BUJORA Mwanza.                 Makumbusho ya  ka...
  • Tumehuzunika kidogo, Cesc Fabregas
  • Computer System Analyst Grade I (Business Analysis) – One Post - (Re-advertised) E-Government Agency (EGA
    Computer System Analyst Grade I (Business Analysis) – One Post - (Re-advertised) E-Government Agency (EGA) Date Listed: J...
  • Post: Part-time journalist
    Post: Part-time journalist Job Description Timely and accurately collecting African real-time news and then integrate the manuscript ...
  • Tempetation
    An Ivy League-educated marriage counselor who gives marital advice but finds it difficult to address issues with her own marriage.    Jur...
  • University of Dar es Salaam among top 100 Universities in Africa
    The university of Dar-es-Salaam has ranked fourth among top 100 popular universities and higher learning institutions in Africa. This is acc...
  • Admission of Diploma holders into Higher
    TANZANIA COMMISSION FOR UNIVERSITIES Admission of Diploma holders into Higher Education Institutions for the academic year 2013/2014. The T...
  • Community Relations Manager – (One Post)
    Community Relations Manager – (One Post) African Barrick Gold (ABG) Date Listed: May 15, 2013 Email Address: ...
  • Kim Kardashian awateka tena mashabiki kwa mavazi
    Kim Kardashian aliweza tena kuuteka umati waliohudhuria katika sherehe za kuchangisha fedha kwa ajili ya mfuko wa kuchangisha fedha kwa ajil...

Categories

  • Africa (1)
  • Announcement (13)
  • Biashara (17)
  • Breaking News (4)
  • Burudani (11)
  • East Africa News (19)
  • Education (12)
  • Entertainment (8)
  • Fashions (1)
  • Habari (41)
  • Health (1)
  • International News (14)
  • Jamii (11)
  • Jobs (120)
  • Latest Sports News (3)
  • Local News (59)
  • Makala (8)
  • Michezo (25)
  • Music (5)
  • News (12)
  • Scholarships (4)
  • Scholarships- Jobs (7)
  • Siasa (1)
  • Sport (64)
  • sports (18)
  • Technology (2)
  • Tetesi za Usajili (9)
  • usajili (1)

Blog Archive

  • ▼  2013 (335)
    • ►  September (9)
    • ▼  August (18)
      • USAJILI WA GARETH BALE KWENDA REAL MADRID WAIVA
      • Chelsea join race for Willian,Bale's Madrid move i...
      • Maeneo ya Dar yakosa umeme baada ya moto kuunguza ...
      • Benki ya Taifa Biashara yazindua kampeni ya kuweka...
      • Real Madrid are rumoured to be holding the number ...
      • Just like OBAMA and OPRAH , Robert Kelly will aslo...
      • Oprah tells her Serengeti trip story through photos
      • Wenger kumgeukia Michu
      • MIWANI PANA YA EDO ~ TATHMINI YA MECHI YA KWANZA Y...
      • University of Dar es Salaam among top 100 Universi...
      • Cristiano Ronaldo's future at Real Madrid remains ...
      • THIAGO ALCANTARA KULETA MZOZO BAYERN!!
      • Clinton atua Dar kiaina
      • Vichwa vya Magazeti leo kuhusu usajili Barani Ulaya
      • REAL MADRID NA MANCHESTER UNITED KWENYE MAZUNGUMZO...
      • Real Madrid stars worried Ronaldo will leave
      • Waziri Mkuu Pinda ashtakiwa mahakamani
      • Waziri Mkuu Pinda ashtakiwa mahakamani
    • ►  July (23)
    • ►  June (27)
    • ►  May (91)
    • ►  April (53)
    • ►  March (41)
    • ►  February (59)
    • ►  January (14)
  • ►  2012 (162)
    • ►  December (42)
    • ►  November (70)
    • ►  October (50)
Powered by Blogger.

About Me

Unknown
View my complete profile