MAKANGALESOPHIE

  • Subscribe to our RSS feed.
  • Twitter
  • StumbleUpon
  • Reddit
  • Facebook
  • Digg

Tuesday, 12 February 2013

Digitali yavunja ndoa za watu uswahilini

Posted on 05:50 by Unknown

Digitali yavunja ndoa za watu uswahilini
. Fumanizi zaongezeka mitaani
.Vijana wengi wakosa bongo flavour na maiigizo
. 40% ya wakazi wa jiji hawatizami Televisheni majumbani
.Wasanii wa kizazi kipya wakosa promo
   “Tangu mfumo wa digitali kuanza katika jiji la Dar es Salaam mahusiano ya wachumba na ndoa nyingi zinaendelea kuvunjika hasa sehemu za uswahilini kwa sababu wachache wenye ving’amuzi wanatumia kama nyenzo ya kupata wanawake hasa kwenye vipindi vinavyopendwa sana na watazamaji wakinamama,” anasema Alban Marcus.

Akizungumza na Clouds Television jijini Dar es Salaam, Bw Marcus ambaye ni Mkurugenzi wa (Citizen Public Watch) anasema huku uswahilini mafumanizi yameongezeka kwa kasi ya ajabu baada ya wenye ving’amuzi kutumia upenyo huo kutembea na wachumba na wake za watu.
Bw Marcus anasema kwamba mfumo wa digitali nchini Tanzania uliharakishwa bila ya kutolewa elimu ya kutosha Kwa wananchi wote Ili waelewe nini maana ya analogia na mfumo mpya wa digitali na manufaa yake kwa watumiaji wa televisheni hapa nchini.

Anasema kutokana na msukumo wa wafanyabiashara ambao wanawaza na kufikiri kibiashara zaidi na kutomdhamini mlaji ambaye ndio mtanzania wa hali ya chini mfumo huu mpya umewaweka pembeni watu wenye kipato cha chini hapa Tanzania.

Katika mfumo wa digitali Serikali ilifanya haraka kuzima bila ya kuwadhamini kwanza wananchi wake hasa wenye vipato vya kati na vya chini na hali ya kiuchumi kwa ujumla kabla ya kuwashirikisha kwa lazima katika mfumo mpya wa teknolojia.

Bw Marcus alisisitiza kwamba mfumo wa digitali ulipaswa uende sambamba na elimu ya teknolojia mpya kwa wananchi lakini cha kushangaza zaidi ni kwamba hata makampuni ya kusambaza ving’amuzi vilikuwa bado havijajipanga kwa mfumo mpya wa matangazo.

“Uhuru na haki ya kupata habari na matangazo upo kitanzini wananchi sasa wanalazimika kununua na kulipia taarifa ya habari na matangazo kwani tunarudi kwenye ujima?

“Kwa hakika mfumo huu hauwezi kuharakisha maendeleo maana upatikanaji wa habari na elimu ya uraia unasambaa kwa urahisi na haraka zaidi kwa njia ya televisheni hata kwenye kuunda mabaraza ya katiba mfumo rahisi wa mawasiliano ni huu wa televisheni,” alisema Marcus 

Wakati wa kuzima mtambo wa digitali ilikuwa ni kipindi cha mwisho wa mwaka kwamba watu wengi wenye hata kipato cha kati walikuwa wanajiandaa na karo za watoto wao mashuleni kwahiyo serikali ilikuwa inatakiwa kutizama hali za kiuchumi za wananchi wake kwa wakati husika.

Ilikuwa Desemba 31, mwaka jana ilikuwa mwisho wa mimi Mtanzania wa kawaida kutizama kipindi cha michezo cha sports bar kinachorushwa na Clouds TV ambacho ni mmoja wa vipindi bora na vinavyonisisimua sana,” anasema Said Khamis Mkazi wa jiji la Dar es Salaam.

Tanzania ilingia rasmi katika mfumo wa kurushia matangazo ya televisheni kwa njia ya dijitali kutoka katika mfumo wa analogia tangu mwaka katika mkoa mmoja pekee wa Dar es Salaam na kuacha maelfu ya wakazi wa jiji wenye kipato cha chini bila matangazo ya televisheni anasema khamis.

Huo ulikuwa ni usiku wa kuamkia Januari mosi mwaka huu, ambapo mitambo ya analojia ilizimwa na mamlaka husika kwa mkoa huu na kuungana na nchi nyingine duniani zilizotangulia kwenye mfumo wa digitali ili kwa kile kinachoelezwa kutoa picha na sauti nzuri.

Kuja kwa mfumo wa dijitali kulitokana na agizo lililotolewa na Tume ya Kimataifa ya Mawasiliano (ITU) kwa nchi zote duniani kuhamia kwenye mfumo huo ifikapo Julai, 2015.

Nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki, Tanzania imekuwa ya kwanza kutekeleza agizo hilo mapema badala ya kusubiri hadi tarehe ya mwisho iliyowekwa na ITU.

Katika kufanikisha hilo, Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imetoa vibali kwa kampuni tatu kufanya kazi ya usambazaji wa mfumo wa dijitali, ambazo ni Star Media Tanzania Limited (Startimes) yenye ushirikiano na Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) na Star Communications and Technology ya China, Ting ya Agape Associates na Basic Transmissions ya Kampuni za IPP Media pamoja na Sahara Communications.

Kwa kuanzia, TCRA imechagua mikoa saba ambapo imeanza na Mkoa wa Dar es Salaam, huku Dodoma na Tanga ikitarajiwa kuanza Januari 31, Mwanza Februari 28, Moshi na Arusha Machi 31 na Mbeya ni Aprili 30 mwaka huu.

Wakati mikoa mingine ikiendelea kutumia mfumo wa analojia, imeahidiwa ndani ya miezi nane mwaka huu, teknolojia ya dijitali itakuwa imeenea kote.

Lakini siku chache baada ya kuanza kwa mfumo huu mpya jijini Dar es Salaam, tafiti zilizofanywa na TCRA zinaonesha asilimia 90 ya wakazi wake wanatumia mfumo huu.

Mbali ya hilo kumekuwa na malalamiko kwa wakazi wengi wa jiji kuhusu ubora wa huduma za baadhi ya ving’amuzi kuwa havikidhi kiwango kinachotakiwa kulingana na fedha wanazozitoa.

Aidha, wakazi hao wanadai kuwa ving’amuzi hivyo vimekuwa na matatizo ya sauti pamoja na picha hasa kwa wale waliolipia vituo vichache huku wakilalamikia bei za ving’amuzi na vifurushi vyake kuwa kubwa tofauti na vipato vya wengi.

Wakazi hao wanasema kuna mafundi wachache wa kuunganisha ving’amuzi, hivyo ambao pia hawapatikani kiurahisi huku wakisema lugha iliyotumika kutoa maelezo ya jinsi kuunganisha si ya taifa hivyo ni vigumu kwa watu wengi kuelewa.
Wakizungumza na kituo hiki kwa wakati tofauti, wakazi hao wanasema wamekuwa wakipewa namba za watu wa huduma kwa wateja, lakini imekuwa vigumu kuwapata pindi wanapohitaji msaada.
Anitha George, mkazi wa Banana jijini Dar es Salaam anasema mfumo wa dijitali umeleta usumbufu mkubwa sana kwani imekuwa shida kupata matangazo ya televisheni kama zamani.

“Muda mwingi matangazo hayaonekani vizuri huku ukitokea ujumbe wa ‘hakuna huduma’, wakati mwingine matangazo yakiwa yanaendelea picha zikiganda na ikitokea picha ikionekana vizuri basi sauti haitasikika,” anasema Anitha.

Naye Mary Jacob mkazi wa Buguruni, alisema bei za ving’amuzi bado ni tatizo kwa Watanzania walio wengi na kutoa pendekezo kwa serikali kupanga bei stahiki itakayowalinda watu wa hali zote.
“Hizi bei zao hata hazijawalenga wanyonge, kama mtu anashindwa kununua antena ya sh 3,000 (si za ving’amuzi) ataweza kununua king’amuzi cha sh 48,000 kinachohitaji vitu kibao?

“Mimi nadhani serikali ingesimamia hili ili bei iwe hata sh 7,000 watu wanaweza kumudu,” anasema Mary.
Naye Issa Hamad anaeleza kwamba: “Jamani sidhani kama Watanzania wote ni wasomi…nashangaa hivyo vinavyotumika kuelekezea jinsi ya kuunganisha ving’amuzi (menu) vimeandikwa kwa lugha ya Kiingereza.”
Baadhi ya wakazi hao waliitupia lawama serikali kwa kuharakisha kuingia kwenye dijitali wakati mfumo huo ukiwa haujaenea kwenye miji yote nchini na kushangazwa na kila kituo cha televisheni kutangaza king’amuzi chake.

Ving`amuzi vimesaidia kupunguza wimbi la uvivu wa kukesha Tiviini kuangalia maigizo, bongo flavor, wabongo wengi hasa wa uswazi hawawezi kumiliki sh 30000 au 50000 za kununulia ving`amuzi hii ni sawa na kusema Serikali imefanikiwa kupunguza watazama Tv sugu kwa asilimia zaidi ya 40% na haya ndio maendeleo tuyatakayo! Ambokile Msonda

Mwisho.
Email ThisBlogThis!Share to XShare to FacebookShare to Pinterest
Posted in Habari | No comments
Newer Post Older Post Home
View mobile version

0 comments:

Post a Comment

Subscribe to: Post Comments (Atom)

Popular Posts

  • Christiano Ronaldo and His 29 girlfriends List.
    Chr is tiano Ronaldo is famous as a great and cool football player. He play for England Manchester United Club, at age of 26 and he already...
  • Maadhimisho ya miaka 100 ya kituo cha makumbusho ya utamaduni wa Kisukuma - BUJORA Mwanza.
    Maadhimisho ya miaka 100 ya kituo cha makumbusho ya utamaduni wa Kisukuma - BUJORA Mwanza.                 Makumbusho ya  ka...
  • Tumehuzunika kidogo, Cesc Fabregas
  • Computer System Analyst Grade I (Business Analysis) – One Post - (Re-advertised) E-Government Agency (EGA
    Computer System Analyst Grade I (Business Analysis) – One Post - (Re-advertised) E-Government Agency (EGA) Date Listed: J...
  • Post: Part-time journalist
    Post: Part-time journalist Job Description Timely and accurately collecting African real-time news and then integrate the manuscript ...
  • Tempetation
    An Ivy League-educated marriage counselor who gives marital advice but finds it difficult to address issues with her own marriage.    Jur...
  • University of Dar es Salaam among top 100 Universities in Africa
    The university of Dar-es-Salaam has ranked fourth among top 100 popular universities and higher learning institutions in Africa. This is acc...
  • Admission of Diploma holders into Higher
    TANZANIA COMMISSION FOR UNIVERSITIES Admission of Diploma holders into Higher Education Institutions for the academic year 2013/2014. The T...
  • Community Relations Manager – (One Post)
    Community Relations Manager – (One Post) African Barrick Gold (ABG) Date Listed: May 15, 2013 Email Address: ...
  • Kim Kardashian awateka tena mashabiki kwa mavazi
    Kim Kardashian aliweza tena kuuteka umati waliohudhuria katika sherehe za kuchangisha fedha kwa ajili ya mfuko wa kuchangisha fedha kwa ajil...

Categories

  • Africa (1)
  • Announcement (13)
  • Biashara (17)
  • Breaking News (4)
  • Burudani (11)
  • East Africa News (19)
  • Education (12)
  • Entertainment (8)
  • Fashions (1)
  • Habari (41)
  • Health (1)
  • International News (14)
  • Jamii (11)
  • Jobs (120)
  • Latest Sports News (3)
  • Local News (59)
  • Makala (8)
  • Michezo (25)
  • Music (5)
  • News (12)
  • Scholarships (4)
  • Scholarships- Jobs (7)
  • Siasa (1)
  • Sport (64)
  • sports (18)
  • Technology (2)
  • Tetesi za Usajili (9)
  • usajili (1)

Blog Archive

  • ▼  2013 (335)
    • ►  September (9)
    • ►  August (18)
    • ►  July (23)
    • ►  June (27)
    • ►  May (91)
    • ►  April (53)
    • ►  March (41)
    • ▼  February (59)
      • Fergie: Let me move upstairs
      • NBC APPOINTS NEW MANAGING DIRECTOR
      • Tanzania Portland Cement launches new expansion fo...
      • Kenya boy, 13, gains fame for protecting livestock...
      • Do not fight over land, says National Lands Commis...
      • Monetary Boards in collaboration to support develo...
      • Rais Kikwete akagua Ukumbi wa Kisasa wa Mikutano w...
      • ‘Kitanda kimoja wanalazwa watoto 4, mliyoikuta leo...
      • Heart suggery in Tanzania coming Soon...
      • Je huu ndio mwisho wa Ufalme wa Barcelona???
      • Accounts Receivables Manager
      • 2. Chief Operational Officer
      • Youth Civic Engagement Assistant Project Coordinat...
      • Customer Services / Marketing Administrator ? Clot...
      • Kesi dhidi ya Sh. Ponda: Serikali yafunga ushahidi.
      • Gareth Bale Goals 2012/2013
      • Are Spurs a one-man team?
      • Mancini zaidi ya Benitez, Swansea yafanya mauji ko...
      • Beckaham zaidi ya Joe Barton Ufaransa
      • Rafael amazing goal vs QPR 2013 & Man united vs Qpr
      • Ajali mbaya ya mashindano ya Magari yajeruhi watu 33
      • Mil 142/= zapatikana Mama Salma akiongoza hafla ku...
      • Yanga Yaididimiza Azam, Manchester yaendelea kupaa!!!
      • Accountant for Charity
      • Volunteer Accountant for Charity
      • Vibwanga vya Masta wa majuu katika picha
      • Africa Specialist Tailormade Travel Consultant - C...
      • Barcelona Chaliiiii mbele ya Ac Milan
      • The growth rate of world manufacturing output rema...
      • A major progress has been made on the fight agains...
      • Vibwanga vya Mastaa wa Majuu
      • Wanafunzi wajiua kwa kufeli mtihani wa Kidato cha ...
      • SASA MKAZO NI KUMALIZA NAFASI YA 4 BPL!!
      • SASA MKAZO NI KUMALIZA NAFASI YA 4 BPL!!
      • Supermario Balotelli
      • Taarifa ya Katibu wa Bunge.
      • Post: Part-time journalist
      • Oscar Pistorius arrested over fatal shooting
      • Huyu ndiye Mrembo aliyeuawa na Bingwa wa Olympic y...
      • Museveni abuses uniform -Besigye
      • 2 *PhD* Positions in Programming Language-based Se...
      • Job Advert--BBC Worldwide Limited.
      • Analyst/Economist Vacancy
      • Tahadhari kuhusu kupandishwa vyeo kupitia ujumbe w...
      • Digitali yavunja ndoa za watu uswahilini
      • Pope Benedict will Resigns on February 28th, 2013
      • Michezo mbalimbali ya mwishoni mwa wiki! katika Pi...
      • Nigeria Mabingwa wapya wa Africa 2013
      • Baada ya Jamie Caragger kutundika Daluga...wajue w...
      • Master in Leading Innovation and Change from York ...
      • Vibwanga vya mastaaa wa majuu
      • Mwanafunzi wa miaka 9 mbaroni kwa kumwibia mwallim...
      • Drogba 's reaction after papis cisses goal
      • Heavy Equipment Engineers
      • Tanzania 1 Cameroon 0
      • FNB Celebrated one Year in Tanzania
      • TPA and Mombasa Porty Authorithy on mission to cur...
      • Mario Balotelli anza kungaa Italia
      • Maandalizi ya Super Bowl Sunday Yapamba moto
    • ►  January (14)
  • ►  2012 (162)
    • ►  December (42)
    • ►  November (70)
    • ►  October (50)
Powered by Blogger.

About Me

Unknown
View my complete profile