MAKANGALESOPHIE

  • Subscribe to our RSS feed.
  • Twitter
  • StumbleUpon
  • Reddit
  • Facebook
  • Digg

Monday, 25 February 2013

Kesi dhidi ya Sh. Ponda: Serikali yafunga ushahidi.

Posted on 21:36 by Unknown
Imeandikwa na Happiness Katabazi

HATIMAYE upande wa Jjamhuri katika kesi ya uchochezi na kuiba malighafi zenye thamani ya Sh. milioni 59 inayomkabili Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu, Sheikh Ponda Issa Ponda na wenzake 48, umetangaza rasmi kuifunga kesi yake.

Hayo yalisemwa na Wakili Mwandamizi wa Serikali, Tumaini Kweka mbele ya Hakimu Mkazi Victoria Nongwa wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam, muda mfupi baada ya shahidi wa 17 wa upande wa Jamhuru D/C F8586 Ismail wa kituo cha Polisi Chang’ombe kumaliza kutoa ushahidi wake ambapo jana jumla ya mashahidi watatu kwa mpigo walitoa ushahidi wao.

Wakili Kweka alieleza kuwa hadi kufikia jana upande wa  Jamhuri ulikuwa umeleta mashahidi 17 na vielelezo 13 ambavyo vilipokelewa mahakamani kama vielelezo vimetosheleza upande wa Jamhuri kufikia uamuzi huo wa kuifunga kesi yao.

Baada ya wakili Kweka kutoa maelezo hayo wakili wa Ponda, Juma Nassor aliiomba mahakama iwapatie muda hadi Machi 4 ili waweze kwenda kujiandaa na kufanya utafiti utakaowawezesha kuwasilisha maombi ya kuwaona wateja wao wote 49 hawana kesi ya kujibu.

Hata hivyo, Hakimu Nongwa alisema jukumu la kupanga tarehe ya kuja kufanya majumuisho ya mawakili wa pande hizo mbili katika kesi hiyo ya kuwaona washitakiwa wanakesi ya kujibu au la ni vyema ikaachiwa mahakama. Hakimu huyo akatoa amri kuwa majumuisho hayo yatafanyika Februali 27, 2013, saa mbili asubuhi  na kuutaka upande wa utetezi  kuwa wa kwanza kuwasilisha majumuisho yao kwa njia ya mdomo.

Kabla ya Hakimu Nongwa kukubali ombi la upande wa Jamhuri majira ya saa nane mchana, la kuifunga kesi yake, alisikiliza ushahidi wa mashahidi watatu wa waliokuwa wameletwa na upande wa Jamhuri ambao ni shahidi wa 15 ambaye ni F3929 D/C  Constebo Eliaeli (35), shahidi wa 16 ambaye ni Stationi Sajenti  Amos wa kituo cha Polisi Kati na Shahidi wa 17 ambaye ni askari mpelelezi Na. F8586 D/C Ismail.

Kwa upande wake shahidi wa 17, D/C Ismail aeleza mahakama kuwa Oktoba 17 mwaka jana, alipewa kazi na Mkuu wake wa kazi  na saa 2-9 alasiri alikuwa katika kituo cha Polisi Kijinyoma alipewa jukumu la kuwahoji washitakiwa ambao walikamatwa katika kiwanja cha Chang’ombe Marskas  wakikabiliwa na makosa ya kuingia kwa jinai katika kiwanja hicho .

Ismail alidai kuwa yeye alimhoji mshitakiwa aitwaye  Fiswaa ambaye alimweleza kuwa kati ya tarehe, mwezi na saa isiyofahamika akiwa nyumbani kwake Mlandazi Mkoani Pwani, akiwa anasikiliza Redio Iman, alisikia tangazo lilokuwa likiwataka waumini wa dini ya Kiislamu kwenda kuongeza nguvu ya kujenga msikiti katika kiwanja cha Chang’ombe Markas ambacho ni mali ya waislamu na si BAKWATA, lakini kilikuwa kimevamiwa.

Shahidi huyo alidai kuwa, mshitakiwa huyo alimweleza kuwa  aliitikia wito huo na kufunga safari toka nyumbani kwake Mlandizi na kwenda hadi kwenye kiwanja hicho kilichopo Dar es Salaam, na kuungana na wenzake ambapo kiongozi wao aliyekuwa akiwaongoza walipokuwa kwenye kiwanja hicho ni mshitakiwa wa kwanza ambaye ni  Sheikh Ponda.

“Sululu, mapanga vilitumika kama vifaa vya kujengea msikiti wa muda  katika kiwanja hicho  na ndipo usiku wa kuamkia Oktoba 17 mwaka jana, tukiwa tumekaa kwenye kiwanja hicho nikasikia sauti ikisema kuwa panda kwenye gari, panda kwenye gari na sikuwa na kumbukumbuku yoyote...,’ alidai Ismail kuelezwa na Fiswaa. Maelezo ya mshitakiwa huyo yalipokelewa kama kilelezo cha 13 na hakikupingwa na mawakili wa utetezi.

Kwa upande wake shahidi wake Shahidi wa 16, Station Sajenti Amos, alidai kuwa Oktoba 17 mwaka jana alipewa jukumu la kumhoji mshitakiwa Hussein Ally  ambaye mshitakiwa huyo alimweleza kuwa alipokea maelekezo kutoka kwa Masheikh wake wa Msikiti wa Kinyerezi yakimtaka afike katika kiwanja cha Markas na alienda akakutana na wenzake ambapo walianza kufanya usafi  ili waweze kujenga msikiti na walikuwa wakiongozwa na Sheikh Ponda kufanya ujenzi na usafi katika kiwanja hicho ambacho tayari mashahidi wengine kutoka BAKWATA walishasema kiwanja hicho ni mali ya kampuni ya Agritanza Ltd, na siyo BAKWATA tena. Maelezo ya mshitakiwa hayo yalipokelewa kama kielelezo cha 12.

Aidha, shahidi wa 15 , D/C Constebo Elieli  alidai kuwa Oktoba 17 mwaka jana, alipewa jukumu na mkubwa wake wa kazi la kuandika maelezo ya mshitakiwa Mohamed Ramadhan ambaye alimweleza kuwa siku hiyo yeye alikwenda kusali katika eneo la kiwanja hicho akitoa Oysterbay Dar es Salaam. Elieli alieleza kuwa mshitakiwa huyo alimweleza kuwa alifikia uamuzi wa kwenda kusali swala ya alfajiri hapo Chang’ombe Markas kwa sababu alikuwa anauguliwa na ndugu yake anayeishi Keko. Yeye mshitakiwa hakutaka kwenda kuswali Msikiti ya Keko kwa sababu hali ya usalama ilikuwa mbaya na hivyo akaamua kwenda kusali katika eneo hilo la Markas.

“Mshitakiwa huyo akanieleza eti baada ya kusali hapo alfajiri ya Oktoba 17 mwaka jana, ndiyo ghafla alishitukia anakamatwa na mapolisi. Nilipomhoji kama analifahamu vuguvugu la Waislamu kudai haki zao, mshitakiwa huyo alikubali kulifahamu vuguvugu hilo na kwamba yeye pale kwenye lile eneo alipokamatiwa alikuwa katika kutetea  na kudai haki yao ya kurejeshewa kiwanja kile ambacho ni mali ya Waislamu na si BAKWATA,” alidai Elieli. Hata hivyo, mahakama ilikataa kuyapokea maelezo hayo kama kielelezo kwa sababu yana dosari nyingi za kisheria.

Awali Oktoba 18 mwaka jana, ilidaiwa kwa mara ya kwanza mahakamani hapo na wakili Kweka mbele ya Hakimu Nongwa kuwa washitakiwa hao wanakabiliwa na makosa matano likiwemo kosa la kula njama,wizi wa malighafi zenye thamani ya Sh. milioni 59 na uchochezi ambalo linamkabili Ponda na mshitakiwa wa tano, Sheikh Mkadam Swalehe ambao wanaendelea kuzuiliwa gerezani kwa sababu Mkurugenzi wa Mashitaka, DPP, Dk Eliezer Feleshi bado hawajaondolea hati ya kuwafungia dhamana.


Source by www.wavuti.com
Email ThisBlogThis!Share to XShare to FacebookShare to Pinterest
Posted in Habari | No comments
Newer Post Older Post Home
View mobile version

0 comments:

Post a Comment

Subscribe to: Post Comments (Atom)

Popular Posts

  • Christiano Ronaldo and His 29 girlfriends List.
    Chr is tiano Ronaldo is famous as a great and cool football player. He play for England Manchester United Club, at age of 26 and he already...
  • Maadhimisho ya miaka 100 ya kituo cha makumbusho ya utamaduni wa Kisukuma - BUJORA Mwanza.
    Maadhimisho ya miaka 100 ya kituo cha makumbusho ya utamaduni wa Kisukuma - BUJORA Mwanza.                 Makumbusho ya  ka...
  • Tumehuzunika kidogo, Cesc Fabregas
  • Computer System Analyst Grade I (Business Analysis) – One Post - (Re-advertised) E-Government Agency (EGA
    Computer System Analyst Grade I (Business Analysis) – One Post - (Re-advertised) E-Government Agency (EGA) Date Listed: J...
  • Post: Part-time journalist
    Post: Part-time journalist Job Description Timely and accurately collecting African real-time news and then integrate the manuscript ...
  • Tempetation
    An Ivy League-educated marriage counselor who gives marital advice but finds it difficult to address issues with her own marriage.    Jur...
  • University of Dar es Salaam among top 100 Universities in Africa
    The university of Dar-es-Salaam has ranked fourth among top 100 popular universities and higher learning institutions in Africa. This is acc...
  • Admission of Diploma holders into Higher
    TANZANIA COMMISSION FOR UNIVERSITIES Admission of Diploma holders into Higher Education Institutions for the academic year 2013/2014. The T...
  • Community Relations Manager – (One Post)
    Community Relations Manager – (One Post) African Barrick Gold (ABG) Date Listed: May 15, 2013 Email Address: ...
  • Kim Kardashian awateka tena mashabiki kwa mavazi
    Kim Kardashian aliweza tena kuuteka umati waliohudhuria katika sherehe za kuchangisha fedha kwa ajili ya mfuko wa kuchangisha fedha kwa ajil...

Categories

  • Africa (1)
  • Announcement (13)
  • Biashara (17)
  • Breaking News (4)
  • Burudani (11)
  • East Africa News (19)
  • Education (12)
  • Entertainment (8)
  • Fashions (1)
  • Habari (41)
  • Health (1)
  • International News (14)
  • Jamii (11)
  • Jobs (120)
  • Latest Sports News (3)
  • Local News (59)
  • Makala (8)
  • Michezo (25)
  • Music (5)
  • News (12)
  • Scholarships (4)
  • Scholarships- Jobs (7)
  • Siasa (1)
  • Sport (64)
  • sports (18)
  • Technology (2)
  • Tetesi za Usajili (9)
  • usajili (1)

Blog Archive

  • ▼  2013 (335)
    • ►  September (9)
    • ►  August (18)
    • ►  July (23)
    • ►  June (27)
    • ►  May (91)
    • ►  April (53)
    • ►  March (41)
    • ▼  February (59)
      • Fergie: Let me move upstairs
      • NBC APPOINTS NEW MANAGING DIRECTOR
      • Tanzania Portland Cement launches new expansion fo...
      • Kenya boy, 13, gains fame for protecting livestock...
      • Do not fight over land, says National Lands Commis...
      • Monetary Boards in collaboration to support develo...
      • Rais Kikwete akagua Ukumbi wa Kisasa wa Mikutano w...
      • ‘Kitanda kimoja wanalazwa watoto 4, mliyoikuta leo...
      • Heart suggery in Tanzania coming Soon...
      • Je huu ndio mwisho wa Ufalme wa Barcelona???
      • Accounts Receivables Manager
      • 2. Chief Operational Officer
      • Youth Civic Engagement Assistant Project Coordinat...
      • Customer Services / Marketing Administrator ? Clot...
      • Kesi dhidi ya Sh. Ponda: Serikali yafunga ushahidi.
      • Gareth Bale Goals 2012/2013
      • Are Spurs a one-man team?
      • Mancini zaidi ya Benitez, Swansea yafanya mauji ko...
      • Beckaham zaidi ya Joe Barton Ufaransa
      • Rafael amazing goal vs QPR 2013 & Man united vs Qpr
      • Ajali mbaya ya mashindano ya Magari yajeruhi watu 33
      • Mil 142/= zapatikana Mama Salma akiongoza hafla ku...
      • Yanga Yaididimiza Azam, Manchester yaendelea kupaa!!!
      • Accountant for Charity
      • Volunteer Accountant for Charity
      • Vibwanga vya Masta wa majuu katika picha
      • Africa Specialist Tailormade Travel Consultant - C...
      • Barcelona Chaliiiii mbele ya Ac Milan
      • The growth rate of world manufacturing output rema...
      • A major progress has been made on the fight agains...
      • Vibwanga vya Mastaa wa Majuu
      • Wanafunzi wajiua kwa kufeli mtihani wa Kidato cha ...
      • SASA MKAZO NI KUMALIZA NAFASI YA 4 BPL!!
      • SASA MKAZO NI KUMALIZA NAFASI YA 4 BPL!!
      • Supermario Balotelli
      • Taarifa ya Katibu wa Bunge.
      • Post: Part-time journalist
      • Oscar Pistorius arrested over fatal shooting
      • Huyu ndiye Mrembo aliyeuawa na Bingwa wa Olympic y...
      • Museveni abuses uniform -Besigye
      • 2 *PhD* Positions in Programming Language-based Se...
      • Job Advert--BBC Worldwide Limited.
      • Analyst/Economist Vacancy
      • Tahadhari kuhusu kupandishwa vyeo kupitia ujumbe w...
      • Digitali yavunja ndoa za watu uswahilini
      • Pope Benedict will Resigns on February 28th, 2013
      • Michezo mbalimbali ya mwishoni mwa wiki! katika Pi...
      • Nigeria Mabingwa wapya wa Africa 2013
      • Baada ya Jamie Caragger kutundika Daluga...wajue w...
      • Master in Leading Innovation and Change from York ...
      • Vibwanga vya mastaaa wa majuu
      • Mwanafunzi wa miaka 9 mbaroni kwa kumwibia mwallim...
      • Drogba 's reaction after papis cisses goal
      • Heavy Equipment Engineers
      • Tanzania 1 Cameroon 0
      • FNB Celebrated one Year in Tanzania
      • TPA and Mombasa Porty Authorithy on mission to cur...
      • Mario Balotelli anza kungaa Italia
      • Maandalizi ya Super Bowl Sunday Yapamba moto
    • ►  January (14)
  • ►  2012 (162)
    • ►  December (42)
    • ►  November (70)
    • ►  October (50)
Powered by Blogger.

About Me

Unknown
View my complete profile