MAKANGALESOPHIE

  • Subscribe to our RSS feed.
  • Twitter
  • StumbleUpon
  • Reddit
  • Facebook
  • Digg

Sunday, 26 May 2013

Jeshi lafanikiwa kudhibiti vurugu Mtwara

Posted on 02:02 by Unknown
Shughuli za mauzo na manunuzi zilirejea rasmi jana mjini Mtwara, baada ya huduma hizo kusimama kwa siku tatu kutokana na vurugu zilizotokea kuanzia Alhamisi baada ya kusomwa hotuba ya Wizara ya Nishati na Madini na wana-Mtwara kubaini kuwa suala lao la gesi halijapewa umuhimu unaostahili. Picha na Abdallah Bakari  




Mtwara. 

Mkuu wa vikosi vya aridhini wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), Meja Jenerali SM Kijuu amewahakikishia ulinzi wafanyabiashara hao, baada ya kukutana na uongozi wa Chama cha Wafanyabiashara Sokoni (Wabisoco) jana asubuhi, kufuatia wafanyabishara hao kudai kuendelea kusitisha biashara zao kwa kuhofia usalama.

Katibu wa Wabisoco, Saidi Namata ameliambia Mwananchi Jumapili kuwa wafanyabiashara hao wamekubaliana kufungua biashara zao, baada ya makubaliano ya kulinda eneo hilo na askari wa JWTZ.

“Sisi wafanyabiashara tulikuwa tayari kuendelea kusitisha huduma kutokana na hali ya usalama kuwa mbaya, alipokuja kiongozi wa jeshi na kutuhakikishia kuwa dhamana ya ulinzi itakuwa chini yao tulikubaliana,” alisema Namata

Alisisitiza: “Kama ulinzi ungekuwa mikononi mwa polisi, katu tusingefungua. Polisi wenyewe ndiyo hawa wanaovunja maduka na kuiba, kwa kuwa dhamana hii imebebwa na wanajeshi hatuna shaka, tunaomba wafanyabiashara wengine wafungue biashara zao.”

Tangu juzi magari ya matangazo yamekuwa yakipita mjini Mtwara na kuwatangazia wananchi kuendelea na kazi zao kama kawaida kwa kuwa ulinzi umeimarika, huku askari wa JKT na JWTZ waliosheheni silaha wakizunguka mitaani.

Pinda awasili Mtwara

Wakati tukiewnda mitamboni Waziri Mkuu Mizengo Pinda amewasili Mtwara jana jioni na kukutana na viongozi wa mkoa.

Bungeni Dodoma

Suala la mgawanyo wa rasilimali za taifa jana liliendelea kutikisa Bunge, baada ya baadhi yao kueleza kuwa ni haki kwa maeneo yanakotoka rasilimali hizo kunufaika kwanza kabla ya maeneo mengine.

Wakati wabunge hao wakieleza hayo, wengine wamesisitiza kuwa kwa kuwa nchi ni moja Tanzania, rasilimali zote ni mali ya Watanzania wote.

Wabunge wanaotaka rasilimali zinufaishe kwanza maeneo zinakotoka. Wanasema pamoja na ukweli kwamba Tanzania ni moja, watu hao wana haki ya msingi kupata huduma hizo kwanza kuliko wengine.

Mbunge wa Msalala (CCM), Ezekiel Maige alisema anashangaa kwa nini fomula ya rasilimali kuyaendeleza maeneo iliyopatikana, inatumika kwenye Idara ya Wanyamapori na haitumiki katika sekta ya nishati na madini.

“Wananchi walichosema rasilimali tugawane mrabaha. Zinufaishe wao kwanza. Kwenye wanyamapori, tunafanya hivyo kwa nini kwenye madini tunasema taifa litagawanyika? Alihoji.

Maige alisema Tume ya Bomani ilishauri kuwa asilimia 40 ya mapato itumike kuendeleza maeneo ilikopatikana rasilimali hizo na asilimia 60 zikaendeleze maeneo mengine, lakini ushauri huo haufanyiwi kazi.

Mbunge wa Mpanda (Chadema) Said Arfi alitaka hekima kutamalaki katika suala la mgororo wa gesi Mtwara ili taifa iendelee kuwa na hali ya amani na utulivu

“Naishauri Serikali wawashirikishe wananchi katika mambo yanayohusu mustakabali wa maendeleo yao. Elimu ya kutosha ingalikuwapo na ushirikishwa ulio mpana, tusingalifika hapa. Kadiri tunavyochelewa kulitatua tatizo hili, ndivyo tunavyorudi nyuma katika maendeleo,” alisema.

Kwa upande wake Mbunge Mlalo (CCM), Hassan Ngwilizi, alisema anaunga mkono msimamo wa Rais Jakaya Kikwete kuwa rasilimali za taifa ni mali ya Watanzania wote, hivyo ni mwafaka kwa watu kudhani kuwa wanastahili kunufaika na rasimali kwa sababu zimetoka kwao.

“Wale wote wanaofikiri kuleta chokochoko, wajue nchi hii inavyo vyombo vya dola. Kinachowatokea au kuweza kuwatokea, wajilaumu wenyewe,” alisema Ngwilizi na kusisitiza;

Hamad Ali Hamad (CUF) alisema gesi iliyopatikana Mtwara isiwe laana bali ionekane kama baraka. “Serikali ikazungumze na watu wa Mtwara na hili naomba serikali msione tunafanya jambo baya. hakuna lisilozungumzika,” alisema.

Christopher Ole Sendeka wa Simanjiro (CCM) alisema: “Amani ya Tanzania ni tunu isiyoweza kuchezewa na mtu yeyote yule na kwa sababu yeyote ile .

“Natambua kuna haja ya baadhi ya mambo wanayodai kuangaliwa kwa makini, lakini nawashauri Wanamtwara waendelee kuleta madai yao na Serikali iwasikilize kwa sababu wao ni watu wazima, hawawezi kupiga kelele hivi hivi tu,” alisema.

Ole Sendeka alitaka Waziri asikubali kuendelea kudanganywa na watalaamu wake kwa kuwa watamharibia.

“Usikubali kuuziwa mbuzi kwenye gunia,” alisema Sendeka na kuendelea, “ mwaka jana ulidanganywa na watalaamu wako ukalidanganya Bunge kuhusu nguzo za Tanesco na misumari.”

“Mwaka 2010 Rais Kikwete aliahidi kuwapa mgodi wa Tanzanite One wachimbaji wadogo lakini leo tunaambiwa wakifunga, mgodi huo utakabidhiwa kwa Stamico. Sasa Rais Ni Muhongo au Dk Jakaya Kikwete?”

Kamati yaundwa

Bunge limeunda kamati maalumu kwa ajili ya kuchunguza vurugu zilizotokana na mradi wa kusafirisha gesi, kutoka mkoani Mtwara kwenda jijini Dar es Salaam.

Spika wa Bunge Anne Makinda, alisema kamati hiyo itakayoongozwa na Mbunge wa Muleba Kaskazini, Charles Mwijage, itakuwa na hadidu nne za rejea. 

Wajumbe wake ni Mbunge wa Mpanda Mjini, (Chadema) Said Arfi , Mbunge wa  Sikonge (CCM), Said Nkumba, Mbunge wa Wawi (CUF) Hamad Rashid Mohamed na Mbunge wa Tunduru Kaskazini (CCM) Ramo Makani na Rukia Kassim Ahmed (CCM).

Pia wamo Dk Dalaly Kafumu (CCM-Igunga), Cynthia Hilda Ngoye (Viti Maalumu-CCM), Muhamed Chombo (CCM), Agripina Buyogera NCCR- Mageuzi, Cecilia Paresso (Viti Maalumu-Chadema), Mariam Kisangi (Viti Maalumu- CCM), Seleman Jafo (Kisarawe CCM),

Hadidu za Rejea      
                                     

Spika Makinda alisema kamati hiyo ambayo hata hivyo hakuipa muda maalumu, itakuwa na jukumu la kufuatilia mambo manne muhimu yanayochangia vurugu hizo.

“Kamati itakuwa na jukumu la kujua nini chanzo cha vurugu, kujua hatua zilizochukuliwa na Serikali, kukutana na wadau mbalimbali ili kupata maoni yao na kuangalia mambo yote yenye uhusiano na vurugu hizo,” alisema.
Imeandikwa na Abdallah Bakari, Elias Msuya , Mtwara na Kizitto Noya, Dodoma

Habari hii imenukuliwa kutoka gazeti la mwananchi




























Email ThisBlogThis!Share to XShare to FacebookShare to Pinterest
Posted in Habari | No comments
Newer Post Older Post Home
View mobile version

0 comments:

Post a Comment

Subscribe to: Post Comments (Atom)

Popular Posts

  • Christiano Ronaldo and His 29 girlfriends List.
    Chr is tiano Ronaldo is famous as a great and cool football player. He play for England Manchester United Club, at age of 26 and he already...
  • Maadhimisho ya miaka 100 ya kituo cha makumbusho ya utamaduni wa Kisukuma - BUJORA Mwanza.
    Maadhimisho ya miaka 100 ya kituo cha makumbusho ya utamaduni wa Kisukuma - BUJORA Mwanza.                 Makumbusho ya  ka...
  • Tumehuzunika kidogo, Cesc Fabregas
  • Computer System Analyst Grade I (Business Analysis) – One Post - (Re-advertised) E-Government Agency (EGA
    Computer System Analyst Grade I (Business Analysis) – One Post - (Re-advertised) E-Government Agency (EGA) Date Listed: J...
  • Post: Part-time journalist
    Post: Part-time journalist Job Description Timely and accurately collecting African real-time news and then integrate the manuscript ...
  • Tempetation
    An Ivy League-educated marriage counselor who gives marital advice but finds it difficult to address issues with her own marriage.    Jur...
  • University of Dar es Salaam among top 100 Universities in Africa
    The university of Dar-es-Salaam has ranked fourth among top 100 popular universities and higher learning institutions in Africa. This is acc...
  • Admission of Diploma holders into Higher
    TANZANIA COMMISSION FOR UNIVERSITIES Admission of Diploma holders into Higher Education Institutions for the academic year 2013/2014. The T...
  • Community Relations Manager – (One Post)
    Community Relations Manager – (One Post) African Barrick Gold (ABG) Date Listed: May 15, 2013 Email Address: ...
  • Kim Kardashian awateka tena mashabiki kwa mavazi
    Kim Kardashian aliweza tena kuuteka umati waliohudhuria katika sherehe za kuchangisha fedha kwa ajili ya mfuko wa kuchangisha fedha kwa ajil...

Categories

  • Africa (1)
  • Announcement (13)
  • Biashara (17)
  • Breaking News (4)
  • Burudani (11)
  • East Africa News (19)
  • Education (12)
  • Entertainment (8)
  • Fashions (1)
  • Habari (41)
  • Health (1)
  • International News (14)
  • Jamii (11)
  • Jobs (120)
  • Latest Sports News (3)
  • Local News (59)
  • Makala (8)
  • Michezo (25)
  • Music (5)
  • News (12)
  • Scholarships (4)
  • Scholarships- Jobs (7)
  • Siasa (1)
  • Sport (64)
  • sports (18)
  • Technology (2)
  • Tetesi za Usajili (9)
  • usajili (1)

Blog Archive

  • ▼  2013 (335)
    • ►  September (9)
    • ►  August (18)
    • ►  July (23)
    • ►  June (27)
    • ▼  May (91)
      • Real Madrid yapatwa na kigugumizi
      • Parallel institutions vital to monitor tax adminis...
      • Agents told to exploit opportunities in insurance ...
      • Sida dishes out USD 10m to support agricultural gr...
      • Medical in Charge Emergency Medical Department Muh...
      • Office Administrator
      • Mourinho arudi zake Chelsea, Bale kuuzwa kwa paund...
      • Robin van Persie shows amazing skills v kids....
      • The Government has been urged to protect local in...
      • Dar es Salaam Goat Races to take part on 1st June ...
      • Jeshi lafanikiwa kudhibiti vurugu Mtwara
      • Neymar amua kuelekea Barcelona
      • Bayern Munich Mabingwa wapya wa Ulaya, Neymar aele...
      • Adnan Januzaj - Manchester United 2013
      • Dar Looks Forward to Obama's Tour
      • African Must Improve Livestock Data
      • Safari lager beer wins top Africa awards
      • Polisi kawe wabambikizia watu kesi
      • The implementation of 400 MW gas-fired power proje...
      • Kenyan celebrities at MTV All stars’ red carpert
      • HARUNA NIYONZIMA ASAINI MIAKA MIWILI YANGA SC
      • Bingwa wa Europa kuingia mojamoja Champions Ligi k...
      • Mtwara: Askari watuhumiwa kubaka, kumwua mjamzito,...
      • Kocha wa Malaga, Manuel Pellegrini kubwaga manyang...
      • Maonyesha ya 8 ya Vyuo Vikuu ya TCU yaanza rasmi j...
      • Picha za Mpambano baina ya Yanga na Simba
      • Torres kufungashiwa virago vyake dirisha la usajili
      • Zantel rewards winners of ‘Recharge and Win’ promo...
      • This week Sports on The Rumor Mill
      • Kandoro apongeza ushindi Safari Lager
      • Alex Ferguson's final Press conference
      • OMBI KWA MHE RAIS JAKAYA KIKWETE OKOA ARDHI YETU N...
      • BSL Interpreter / Tanzanian Orphanage
      • Linah, Barnaba kutimuliwa THT
      • Weigh Bridge Operators (3 Posts)
      • Administrative Assistant
      • David Beckhma hatiamye atundika daluga rasmi....
      • Sales Officers with AKIBA Commercial Bank PLC.
      • Bank Tellers Vacancy Posts
      • Community Relations Manager – (One Post)
      • Bookings and Marketing Officer
      • Vodacom na Samsung zazindua S4 nchini Tanzania
      • Angelina Jolie akatwa matiti kuzuia Saratani
      • Beckham aweka Rekodi mpya
      • Man Utd lift Premier League trophy
      • Ngono zembe ilivyokithiri barabara ya kuelekea Zambia
      • Roberto Mancini atolewa nishai na Roberto mwenzake
      • Mariah Carey - #Beautiful ft. Miguel
      • David Moyes, kocha mpya wa Mabingwa wa Uingereza a...
      • Finance Manager-ActionAid Tanzania
      • Operation Supervisors-Tanzania International Conta...
      • Monitoring and Evaluation Officer
      • Financial Controller
      • Human Resources and Administration Officer
      • Tanzania has a long bilateral relations with Arabs
      • Goat charity races to raise billions for community...
      • Youth jobs’ gains wiped out by slow recovery
      • AJIRA KWA VIJANA ZAATHIRIWA NA UKUAJI MDOGO WA UC...
      • Donors pledged Tsh 800bn in the general budget sup...
      • Sir Alex Fergsuon Angatuka MAnchester United
      • Accounts Officer
      • Accountant(s)-Vacancy
      • Human Resources and Administration Officer
      • ILO report shows why social protection is crucial ...
      • The East African Round Up
      • Afdb organizes pan-African training workshop
      • Competitive private sector a key to economic growth
      • African financial markets launch its website
      • Vodacom, GNLD signs deal to help clients
      • Nini Chanzo cha Tamaa ya Ngono
      • KAULI YA SERIKALI BUNGENI KUHUSU MLIPUKO ULIOTOKEA...
      • Huyu Ndiye Gareth Bale...
      • Mbatia ataka Kawambwa si tu ajiuzulu, bali ikiweze...
      • Workers around the globe divine on decent jobs.
      • CCM top echelons connected to illegal ivory dealing.
      • TPC set aside incentives to motivate its workers
      • TAMKO LA MTANDAO WA WATETEZI WA HAKI ZA BINADAMU (...
      • Mourinho awataka Frank Lampard na John Terry kubak...
      • Assistant F&B Manager
      • Consultant for End Term Evaluation (Tandahimba Com...
      • Accountant
      • Administration Secretary
      • Website Administrator/Customer Care
      • Marketing and Sales personnel.
      • Information Technology Manager
      • Serikali yachukua uamuzi mgumu, yafuta matokeo
      • Real Madrid wamtaka Chicharito kwa Paundi ml 25
      • Maadhimisho ya miaka 100 ya kituo cha makumbusho y...
      • Rapa wa Kriss Kross afariki Dunia jijini Atlanta
      • Discover new ideas, technologies and business oppo...
      • UFALME wA SOKA LA UHISAPNIA WAKARIBIA UKINGONI.
    • ►  April (53)
    • ►  March (41)
    • ►  February (59)
    • ►  January (14)
  • ►  2012 (162)
    • ►  December (42)
    • ►  November (70)
    • ►  October (50)
Powered by Blogger.

About Me

Unknown
View my complete profile