MAKANGALESOPHIE

  • Subscribe to our RSS feed.
  • Twitter
  • StumbleUpon
  • Reddit
  • Facebook
  • Digg

Friday, 3 May 2013

Serikali yachukua uamuzi mgumu, yafuta matokeo

Posted on 23:32 by Unknown
Dodoma/Dar. Serikali imechukua uamuzi mgumu na kuamua kuwafariji wanafunzi waliofeli mitihani ya kuhitimu kidato cha nne mwaka 2012 baada ya kufuta matokeo hayo na kuamua yaandaliwe upya kwa kutumia utaratibu uliotumika mwaka 2011.
Uamuzi huo wa Serikali umetokana na matokeo mabaya ya mitihani huo yaliyosababisha zaidi ya asilimia 60 ya wanafunzi kupata sifuri.


Kutokana na matokeo hayo, Serikali iliunda Tume inayoongozwa na Profesa Sifuni Mchome kuchunguza matokeo hayo ili kupata ufumbuzi wa kudumu.

Muda mfupi baada ya tamko la Serikali, baadhi ya wadau wa elimu wameeleza kufurahishwa na uamuzi huo, huku Chama cha Walimu Tanzania (CWT) kikiikosoa hatua hiyo, kuwa imekiuka sheria na kupora madaraka ya Baraza la Mitihani Tanzania (Necta).

Akitoa kauli ya Serikali bungeni kuhusu taarifa ya awali ya Tume ya Taifa ya Kuchunguza Matokeo ya Mtihani wa Taifa Kidato cha nne mwaka 2012 jana, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Uratibu na Bunge), William Lukuvi alisema wameagiza Necta kuweka viwango ili matokeo ya wanafunzi yalingane na juhudi zao.

“Standardization ifanyike ili matokeo ya wanafunzi yalingane na juhudi wazizoziweka katika kusoma kwa mazingira, hali halisi ya Tanzania na uamuzi wa taifa kuongeza idadi ya shule na wanafunzi wakati uwekezaji katika ubora unaendelea,” alisema Lukuvi.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge), William Lukuvi, akiwasilisha kauli ya serikali Bungeni Dodoma jana kuhusu taarifa ya awali ya Tume ya Taifa ya kuchunguza matokeo ya mtihani wa taifa wa Kidato cha nne wa mwaka 2012. Picha na Edwin Mjwahuzi 

Lukuvi alisema Necta imeelekezwa kuwa licha ya sheria ya kuanzishwa kwake kuruhusu kufanya marekebisho ya mchakato wa mtihani, marekebisho yoyote ya kubadilisha utaratibu wa kupanga viwango vya ufaulu na madaraja ya mitihani yanatakiwa yahusishe wadau wote wanaohusika na mitalaa, ufundishaji na mtihani.

“Wakati Tume inaendelea kukamilisha kazi yake, uamuzi wa Necta kutumia utaratibu mpya wa kupanga viwango vya ufaulu na madaraja ya matokeo ya mitihani uliotumika 2012 usitishwe,” alisema Lukuvi na kuongeza:

“Badala yake Necta itumie utaratibu uliotumika mwaka 2011 kwa kidato cha nne na sita kwa mitihani yote, ikiwamo utaratibu wa Standardization na kutoa matokeo mapya kwa kuzingatia maelekezo haya.”

Pia, Serikalli imeagiza mchakato wa tuzo wa taifa (National Qualifications Framework) na Mfumo wa Kutahiniwa/ kuthamini maendeleo ya mwanafunzi masomo yake (National Assessment Framework) ukamilishwe haraka iwezekanavyo.

Katika mtihani wa mwaka 2012, wanafunzi 367,756 walifanya mtihani huo na waliofaulu ni 126,847. Waliofaulu kwa kwa madaraja ya kwanza hadi la tatu ni 23,520 sawa na asilimia 6.4 na daraja la nne ni 103,327 sawa na asilimia 28.1, huku 240,909 ambao ni asilimia 65.5 wakipata daraja sifuri.

 Kauli ya CWT

Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Walimu Tanzania (CWT), Ezekiel Oluoch alisema Baraza la Mawaziri limepora kazi za Bodi ya Baraza la Mitihani kwani ndio yenye jukumu la kufuta matokeo kisheria.

Mbali na hilo Oluoch alisema bado wanafanya utafiti ili kuona kama Baraza la Mawaziri lina uwezo wa kufuta matokeo na kuamuru mitihani isahihishwe upya, badala ya Bodi ya Baraza la Mitihani.

Oluoch aliyesema tamko rasmi la CWT kuhusu uamuzi huo wa Serikali litatolewa wiki ijayo, alieleza kuwa kwa sasa wanachunguza kuona kama jambo hilo lina usahihi kwa kiasi gani.

“Mitihani iliyofutwa ilitolewa na Bodi ya Necta ambayo ndio itakuwa na jukumu la kusimamia usahihishaji mpya na kutangaza tena matokeo.

Kama hali yenyewe ndio hiyo ni wazi kuwa haina tena uwezo wa kusimamia jambo hilo, inatakiwa kung’oka na kuundwa bodi mpya,” alisema Oluoch na kuongeza;

“Nasema hivyo kwa sababu hawawezi kula matapishi yao kwa kuwa wao ndio wenye mamlaka ya kutoa tena matokeo hayo na walishasema kuwa yalikuwa mabaya, sasa uzuri wake utatoka wapi tena.”

Alisema kuwa kufutwa kwa matokeo hayo kunaonesha wazi kuwa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi imeshindwa kazi ya kusimamia elimu nchini.

“Pia katika utangazaji wa matokeo anatakiwa waziri mpya wa kufanya hivyo kwa kuwa huyu wa sasa alieleza sababu za wanafunzi kufeli, sasa akiwa anatangaza matokeo mapya atatueleza nini,” alihoji.

Sababu za matokeo mabaya

Waziri Lukuvi alisema takwimu zinaonyesha kushuka kwa ufaulu huo unahusu shule zote na asilimia kwenye mabano, shule za wananchi (1.82); Shule za umma yaani kongwe (6.43); Binafsi (6.39) na Seminari (7.29).

Kuhusu matokeo ya kidato cha nne 2012, Lukuvi alisema tume imebaini licha ya wanafunzi kuwa kwenye mazingira yanayofanana na wenzao waliopita, ufanisi umekuwa ukishuka kwa sababu mbalimbali.

“Ufaulu wao umeshuka zaidi kwa sababu ya mabadiliko ya mchakato wa kuandaa na kutoa matokeo ya mtihani mwaka 2012, mfumo uliotumika kupanga matokeo na madaraja ni tofauti na ule uliotumika miaka iliyotangulia,” alisema Lukuvi na kuongeza:


“Uchunguzi unaonyesha kuwa mwaka 2011, Necta lilikuwa linachakata alama za mwisho kwa kutumia mfumo ambao ulikuwa unabadilika kutegemea hali ya ufaulu kwa mwanafunzi ambao ni National Mean Difference (NMD).

Alisema uataribu huo ulitokana na tofauti ya wastani wa kitaifa wa alama za maendeleo, kutoka alama ya maendeleo endelevu (Continued Assessment-CA) za watahiniwa wote na wastani wa kitaifa wa ufaulu wa mtihani wa mwisho kwa somo husika.

Aliendelea kuwa kila mtahiniwa aliongezewa NMD iliyokokotolewa kwenye alama za mtihani wa mwisho, ili kupata alama itakayotumika kupada daraja la ufaulu.

“Lakini mwaka 2012 lilitumia mfumo mpya wa kuwa na viwango maalumu vya kutunuku (Fixed Grade Range). Tume imebaini kwamba licha ya mfumo huo ulioandaliwa kwa nia nzuri, utaratibu huo mpya hakufanyiwa utafiti wa maandalizi ya kutosha kabla ya kutumika,” alisema.

Lukuvi alisema taarifa ya awali ya tume, inaonyesha kutokana na uchunguzi uliofanyika kwa muhtasari imebaini mambo mbalimbali.

Alisema matokeo ya  kidato cha nne kuanzia mwaka 2008 yamekuwa na mserereko wa kushuka tofauti na miaka iliyotangulia, kwa sababu ya changamoto zinazotokana na mafanikio yaliyopo sasa ya kuongezeka kwa idadi ya shule za msingi na sekondari, hususan mwaka 2011 na 2013 hivyo kuwa na idadi kubwa ya wanafunzi.

“Mwaka 1961 hadi 2011 idadi ya wanafunzi kwa shule za msingi imeongezeka kutoka 486,470 hadi 4,875,764, sawa na ongezeko la wanafunzi 4,389,294 kwa takriban miaka 40,” alisema.

Alisema wanafunzi wameongezeka kutoka 4,875,764 mwaka 2001 hadi 8,247,472 mwaka 2012, sawa na ongezeko la wanafunzi 3,371,708 kwa kipindi cha miaka 11.

Sekondari wanafunzi wameongezeka kutoka 11,832 mwaka 1961 hadi 289,699 mwaka 2001 sawa na ongezeko la wanafunzi 274,867 kwa miaka 40.

Lukuvi alisema kati ya mwaka 2001 hadi 2012 wanafunzi wameongezeka kutoka 289,699 hadi 1,884,270 sawa na ongezeko la watu 1,594,571.

Tume hiyo imebaini changamoto nyingine ni mazingira yasiyo ya kuridhisha ya kufundishia na kujifunzia, ikiwamo upungufu wa miundombinu muhimu ya shule; madarasa, madawati, maktaba, nyumba za walimu, bweni na majengo mengine muhimu.

“Kuna tatizo la uhaba wa walimu, vitabu, zana za kufundishia na matatizo ya ukaguzi wa shule. Vilevile tumebaini Mfumo wa Elimu ya Msingi na Sekondari unakabiliwa na changamoto nyingine mbalimbali ambazo taifa linapitia kwa sasa,” alisema Lukuvi na kuongeza:


 “Yapo masuala ya sera, sheria, mfumo, muundo na changamoto za uhaba wa rasilimali fedha na watu. Tume inaendelea kufanyia kazi maeneo haya kwa kushirikiana na wataalamu na wadau wengine.”

 Habari kwa msaada wa Gazetui la kila siku la Mwananchi

http://www.mwananchi.co.tz/habari/Kitaifa/-/1597296/1841582/-/item/3/-/s03mvmz/-/index.html 


























Email ThisBlogThis!Share to XShare to FacebookShare to Pinterest
Posted in Local News | No comments
Newer Post Older Post Home
View mobile version

0 comments:

Post a Comment

Subscribe to: Post Comments (Atom)

Popular Posts

  • Christiano Ronaldo and His 29 girlfriends List.
    Chr is tiano Ronaldo is famous as a great and cool football player. He play for England Manchester United Club, at age of 26 and he already...
  • Maadhimisho ya miaka 100 ya kituo cha makumbusho ya utamaduni wa Kisukuma - BUJORA Mwanza.
    Maadhimisho ya miaka 100 ya kituo cha makumbusho ya utamaduni wa Kisukuma - BUJORA Mwanza.                 Makumbusho ya  ka...
  • Tumehuzunika kidogo, Cesc Fabregas
  • Computer System Analyst Grade I (Business Analysis) – One Post - (Re-advertised) E-Government Agency (EGA
    Computer System Analyst Grade I (Business Analysis) – One Post - (Re-advertised) E-Government Agency (EGA) Date Listed: J...
  • Post: Part-time journalist
    Post: Part-time journalist Job Description Timely and accurately collecting African real-time news and then integrate the manuscript ...
  • Tempetation
    An Ivy League-educated marriage counselor who gives marital advice but finds it difficult to address issues with her own marriage.    Jur...
  • University of Dar es Salaam among top 100 Universities in Africa
    The university of Dar-es-Salaam has ranked fourth among top 100 popular universities and higher learning institutions in Africa. This is acc...
  • Admission of Diploma holders into Higher
    TANZANIA COMMISSION FOR UNIVERSITIES Admission of Diploma holders into Higher Education Institutions for the academic year 2013/2014. The T...
  • Community Relations Manager – (One Post)
    Community Relations Manager – (One Post) African Barrick Gold (ABG) Date Listed: May 15, 2013 Email Address: ...
  • Kim Kardashian awateka tena mashabiki kwa mavazi
    Kim Kardashian aliweza tena kuuteka umati waliohudhuria katika sherehe za kuchangisha fedha kwa ajili ya mfuko wa kuchangisha fedha kwa ajil...

Categories

  • Africa (1)
  • Announcement (13)
  • Biashara (17)
  • Breaking News (4)
  • Burudani (11)
  • East Africa News (19)
  • Education (12)
  • Entertainment (8)
  • Fashions (1)
  • Habari (41)
  • Health (1)
  • International News (14)
  • Jamii (11)
  • Jobs (120)
  • Latest Sports News (3)
  • Local News (59)
  • Makala (8)
  • Michezo (25)
  • Music (5)
  • News (12)
  • Scholarships (4)
  • Scholarships- Jobs (7)
  • Siasa (1)
  • Sport (64)
  • sports (18)
  • Technology (2)
  • Tetesi za Usajili (9)
  • usajili (1)

Blog Archive

  • ▼  2013 (335)
    • ►  September (9)
    • ►  August (18)
    • ►  July (23)
    • ►  June (27)
    • ▼  May (91)
      • Real Madrid yapatwa na kigugumizi
      • Parallel institutions vital to monitor tax adminis...
      • Agents told to exploit opportunities in insurance ...
      • Sida dishes out USD 10m to support agricultural gr...
      • Medical in Charge Emergency Medical Department Muh...
      • Office Administrator
      • Mourinho arudi zake Chelsea, Bale kuuzwa kwa paund...
      • Robin van Persie shows amazing skills v kids....
      • The Government has been urged to protect local in...
      • Dar es Salaam Goat Races to take part on 1st June ...
      • Jeshi lafanikiwa kudhibiti vurugu Mtwara
      • Neymar amua kuelekea Barcelona
      • Bayern Munich Mabingwa wapya wa Ulaya, Neymar aele...
      • Adnan Januzaj - Manchester United 2013
      • Dar Looks Forward to Obama's Tour
      • African Must Improve Livestock Data
      • Safari lager beer wins top Africa awards
      • Polisi kawe wabambikizia watu kesi
      • The implementation of 400 MW gas-fired power proje...
      • Kenyan celebrities at MTV All stars’ red carpert
      • HARUNA NIYONZIMA ASAINI MIAKA MIWILI YANGA SC
      • Bingwa wa Europa kuingia mojamoja Champions Ligi k...
      • Mtwara: Askari watuhumiwa kubaka, kumwua mjamzito,...
      • Kocha wa Malaga, Manuel Pellegrini kubwaga manyang...
      • Maonyesha ya 8 ya Vyuo Vikuu ya TCU yaanza rasmi j...
      • Picha za Mpambano baina ya Yanga na Simba
      • Torres kufungashiwa virago vyake dirisha la usajili
      • Zantel rewards winners of ‘Recharge and Win’ promo...
      • This week Sports on The Rumor Mill
      • Kandoro apongeza ushindi Safari Lager
      • Alex Ferguson's final Press conference
      • OMBI KWA MHE RAIS JAKAYA KIKWETE OKOA ARDHI YETU N...
      • BSL Interpreter / Tanzanian Orphanage
      • Linah, Barnaba kutimuliwa THT
      • Weigh Bridge Operators (3 Posts)
      • Administrative Assistant
      • David Beckhma hatiamye atundika daluga rasmi....
      • Sales Officers with AKIBA Commercial Bank PLC.
      • Bank Tellers Vacancy Posts
      • Community Relations Manager – (One Post)
      • Bookings and Marketing Officer
      • Vodacom na Samsung zazindua S4 nchini Tanzania
      • Angelina Jolie akatwa matiti kuzuia Saratani
      • Beckham aweka Rekodi mpya
      • Man Utd lift Premier League trophy
      • Ngono zembe ilivyokithiri barabara ya kuelekea Zambia
      • Roberto Mancini atolewa nishai na Roberto mwenzake
      • Mariah Carey - #Beautiful ft. Miguel
      • David Moyes, kocha mpya wa Mabingwa wa Uingereza a...
      • Finance Manager-ActionAid Tanzania
      • Operation Supervisors-Tanzania International Conta...
      • Monitoring and Evaluation Officer
      • Financial Controller
      • Human Resources and Administration Officer
      • Tanzania has a long bilateral relations with Arabs
      • Goat charity races to raise billions for community...
      • Youth jobs’ gains wiped out by slow recovery
      • AJIRA KWA VIJANA ZAATHIRIWA NA UKUAJI MDOGO WA UC...
      • Donors pledged Tsh 800bn in the general budget sup...
      • Sir Alex Fergsuon Angatuka MAnchester United
      • Accounts Officer
      • Accountant(s)-Vacancy
      • Human Resources and Administration Officer
      • ILO report shows why social protection is crucial ...
      • The East African Round Up
      • Afdb organizes pan-African training workshop
      • Competitive private sector a key to economic growth
      • African financial markets launch its website
      • Vodacom, GNLD signs deal to help clients
      • Nini Chanzo cha Tamaa ya Ngono
      • KAULI YA SERIKALI BUNGENI KUHUSU MLIPUKO ULIOTOKEA...
      • Huyu Ndiye Gareth Bale...
      • Mbatia ataka Kawambwa si tu ajiuzulu, bali ikiweze...
      • Workers around the globe divine on decent jobs.
      • CCM top echelons connected to illegal ivory dealing.
      • TPC set aside incentives to motivate its workers
      • TAMKO LA MTANDAO WA WATETEZI WA HAKI ZA BINADAMU (...
      • Mourinho awataka Frank Lampard na John Terry kubak...
      • Assistant F&B Manager
      • Consultant for End Term Evaluation (Tandahimba Com...
      • Accountant
      • Administration Secretary
      • Website Administrator/Customer Care
      • Marketing and Sales personnel.
      • Information Technology Manager
      • Serikali yachukua uamuzi mgumu, yafuta matokeo
      • Real Madrid wamtaka Chicharito kwa Paundi ml 25
      • Maadhimisho ya miaka 100 ya kituo cha makumbusho y...
      • Rapa wa Kriss Kross afariki Dunia jijini Atlanta
      • Discover new ideas, technologies and business oppo...
      • UFALME wA SOKA LA UHISAPNIA WAKARIBIA UKINGONI.
    • ►  April (53)
    • ►  March (41)
    • ►  February (59)
    • ►  January (14)
  • ►  2012 (162)
    • ►  December (42)
    • ►  November (70)
    • ►  October (50)
Powered by Blogger.

About Me

Unknown
View my complete profile