MAKANGALESOPHIE

  • Subscribe to our RSS feed.
  • Twitter
  • StumbleUpon
  • Reddit
  • Facebook
  • Digg

Sunday, 12 May 2013

Ngono zembe ilivyokithiri barabara ya kuelekea Zambia

Posted on 05:54 by Unknown


Baadhi ya magari ya mizigo yakiwa yameegeshwa katika moja ya vituo vilivyopo kandokando ya Barabara Dar es Salaam- Morogoro yakisubiri kuendelea na safari 


Licha ya kuwa na kiwango kikubwa cha maambukizi ya Ukimwi, Mkoa wa Mbeya bado unatajwa kuwa eneo lililokithiri kwa vitendo vya ngono bila kuwa na tahadhari (ngono zembe).
Dar es Salaam. 

Sababu kubwa ya hali hiyo inaelezwa kuwa ni kuwepo kwa maegesho ya malori ya mizigo yanayoelekea Zambia huku madereva wake wakitajwa kuwa wateja wakubwa wa ngono.
Uchunguzi uliofanywa na Mwananchi Jumamosi katika maeneo yanayotajwa kwa biashara ya ngono yaani Kata ya Igawa na Igurusi, umethibitisha kuwepo kwa vitendo hivyo.
  
Igawa
Akizungumza na mwandishi wetu, mmoja wa madereva wa taxi eneo la Igawa aliyejitambulisha kwa jina la Felix, alisema kuwa kwa sasa biashara hiyo imedorora kwa sababu madereva wa malori wamepunguza kusimama hapo.  
“Zamani ungefika hapa saa hizi ungewakuta barabarani kabisa. Lakini siku hizi, malori yameacha kusimama hapa, ndiyo maana nao wamepungua. Lakini wapo baadhi yao ni wahudumu wa baa,” alisema dereva huyo.
Kwa kuwa muda ulikuwa umekwenda na usafiri usiku ni wa shida, mwandishi aliendelea Kata ya Igurusi kwa ajili ya uchunguzi zaidi.
Igurusi
Ni majira ya saa mbili usiku, baada ya kuchukua chumba kwenye nyumba ya wageni iliyo mbali na barabara kuu, nikarudi kwenye baa moja. Kabla sijaondoka, nikamuuliza mama mwenye gesti kama naweza kuleta mwanamke wa kulala naye. Akanijibu kuwa ni uamuzi wangu kwani haizuiwi.
Nilipofika katika baa moja iliyo pembeni mwa barabara (jina linahifadhiwa) nilikuwa nikipata kinywaji huku nikiangalia jinsi ya kumpata mtu wa kuzungumza naye kwa kina.
Namjaribu mhudumu mmoja wa baa hiyo kwa kumtongoza, lakini akasema hawezi kutoka na mimi kwa kuwa bado yuko kazini.
Nahamia baa nyingine ng’ambo ya barabara kwa lengo hilohilo. Hapo nakutana na mama mmoja wa makamo, kisha kumweleza shida yangu kwamba natafuta mwanamke wa kulala naye usiku huo.
“Ni kweli hapa wapo kina dada, ukiwataka mnaelewana tu. Mimi mwenyewe ninaye binti yangu ila nimetuma dukani, labda umsubiri. Lakini kama unaona utachelewa, basi nenda baa ya jirani hapo wapo wengi tu,” alisema mama huyo.
Nikaamua kwenda kwenye baa hiyo jirani na hapo nawakuta kina dada wapatao watano, huku wateja wakiwa wachache tu. Nikaagiza soda na kuanza kuinywa taratibu. Bila kupoteza muda nikamuuliza dada aliyeniletea soda (jina linahifadhiwa)  kama naweza kupata mshichana wa kulala naye usiku huo. Mahojiano yetu yakawa hivi
Mhudumu: Hapa wapo wengi tu… wote unaowaona hapa ndiyo kazi zao, sijui unamtaka nani?

Mwandishi: Mimi nakutaka wewe..


Mhudumu: Mh! Sawa lakini ujue bado niko kazini hadi saa tano usiku. Labda unipe Sh5,000 nikalipe kwa meneja ili aniruhusu.

Mwandishi: Hiyo haina shida, kuna gharama nyingine?
Mhudumu: Ndiyo itabidi pia unilipe hela ya penzi, Sh10,000 na Sh5,000 ya kulipia gesti.

Mwandishi: Mh! Mbona kubwa hivyo? Kwani ni lazima tufanyie kwenye gesti ya hapa?

Mhudumu: Hiyo ndiyo bei yetu ya kawaida. Siyo lazima tulale hapa, kama kuna sehemu nyingine twende tu.
Nampa Sh5,000 ya kulipa kwa meneja wake, huku nikimalizia soda yangu. Mara akawa tayari, tukaondoka kuelekea gesti niliyofikia.
Katika gesti hiyo pia kuna baa na sehemu ya chips. Mazungumzo yetu yakaendelea.


Mhudumu: Kwanza uninunulie chips na samaki maana nina njaa sana. Halafu uninunulie na bia.
Mwandishi: Usihofu utakula tu. Lakini bia mimi situmii kwa hiyo itabidi unisamehe kwa leo. Enhee, hebu nijulishe jina lako na kwa nini umeipenda hii kazi ya baa?

Mhudumu: Mimi naitwa…(jina linahifadhiwa), sina muda mrefu sana hapa Igurusi. Nimekuja kutoka Mbeya mjini kwa mama yangu mzazi. Nilimtoroka mama baada ya rafiki yangu kunirubuni.
Mwandishi; Umefikika kidato cha nne?
Mhudumu: Shule sikumaliza mwaka … aah, nilimaliza mwaka juzi, lakini sikufanya vizuri.
Mwandishi: Ulipata divisheni gani?

Mhudumu: Usinikumbushe machungu… nilipata ‘C’ moja tu, nilikuwa shule ya Southern Highland ya Mbeya. Kilichosababisha nishindwe kuendelea na masomo ni kupata mimba na kuzaa mtoto ambaye sasa ana miaka miwili na yuko kwa mama.
Mwandishi: Kumbe una mpenzi, anajua kwamba uko hapa?
Mhudumu: Wala hajui, kwanza tulikorofishana, japo hatujaachana na anamhudumia mtoto wake vizuri tu.
Baada ya chips kuwa tayari nikamwomba tuingie chumbani. Mazungumzo yakaendelea.
Mwandishi: Sasa tule halafu kazi ianze

Mhudumu: Sawa.
Mwandishi: Hivi tukifanya bila kondomu utanifanyia shilingi ngapi?

Mhudumu: Mh! Mimi naogopa kufanya bila kondomu. Si unipe hela tu nikanunue kondomu hapo nje?
Mwandishi: Kwani nikitafuta mwanamke huko nje wa kufanya naye bila kondomu sipati?

Mhudumu: Wapo wengi tu, hata pale baa uliyoniyonitoa, wanawake wanajiuza na wengine wanaletwa pale ni wake za watu wanakuja wakiwa wamejifunika khanga. Kwa ujumla hapa ngono inafanyika mno.
Baada ya mazungumzo kuendelea nikamwambia, basi kama hataki bila kondomu basi na mimi sitaki kufanya. Nikamlipa Sh5,000 kwa kuwa hatujafanya na kumrudisha nilipomtoa ikiwa ni saa tano usiku.
Utafiti wa NIMR
Utafiti uliofanywa na Taasisi ya Utafiti wa Dawa za Binadamu (NIMR) mwaka 2012, kuhusu upatikanaji na matumizi ya kondomu kwenye maeneo yenye maambukizi makubwa ya Ukimwi hasa katika Barabara ya Tanzania na Zambia wilayani Mbarali, umeonyesha kuwapo kondomu kwa asilimia 52 tu.
Akizungumzia utafiti huo, Mtafiti wa Nimr Emmanuel Makundi alisema kuwa Wilaya ya Mbarali ilichaguliwa hasa katika maeneo ya Igawa, Chimala na Igurusi ikiwa ni njia za kuelekea mipaka ya Zambia na Malawi, ambazo zimekithiri kwa vitendo vya ngono.
“Utafiti wetu umebainisha matumizi hafifu ya kondomu katika maeneo yaliyoathirika zaidi na Ukimwi ya kuelekea mpaka wa Zambia,” alisema Makundi.
Madereva wa malori
Akizungumzia suala hilo, Mwenyekiti wa Kamati ya Madereva wa Malori nchini (Chamamata-CMMT), Rocket Matogolo amekiri tabia ya madereva wa malori kujihusisha na vitendo vya ngono wawapo safarini, lakini akasema kuwa hawashirikishwi katika mapambano hayo:
“Tunalifahamu hilo na tunapigana nalo kwa sababu ni janga linalovunja nguvu kazi ya Watanzania. Tulichotarajia kutoka Serikalini na wadau wengine ni kutushirikisha kama ilivyo kwenye polisi jamii kuliko kulihamishia kwenye sekta nyingine wakati wahusika ni sisi.”
Tacaids
Akizungumzia suala hilo, Mratibu wa miradi maalumu wa Tume ya Kudhibiti Ukimwi nchini, Renatus Kihongo anakiri kuwepo kwa tatizo hilo na kusema kuwa tume hiyo imeshaainisha barabara za masafa marefu na kuziwekea vituo vya huduma za Ukimwi.
“Kuna barabara za Dar es Salaam- Tunduma, Dar es Salaam, Kahama, Ngara kwenda Burundi na Rwanda, kuna Dar es Salaam, Arusha kwenda Kenya na ule mpaka wa Horohoro Tanga. Kote huko kuna maeneo ambayo malori huegeshwa na kuna biashara nyingi ikiwemo ya ngono,” anasema Kihongo.
Anaongeza kuwa Tacaids imefanya tafiti kubaini tatizo hilo ikishirikiana na Tume ya Kudhibiti Ukimwi ya Kenya (NACC) na Shirika la Uhamiaji la Kimataifa (IOM).
Anasema kuwa katika utafiti huo wamepata taarifa za moja kwa moja za tabia za watu, idadi yao na kiwango cha huduma wanachotakiwa kupata.
Anataja pia mkakati unaooanisha shughuli za Ukimwi kwa nchi za Afrika Mashariki, ambapo huduma zake zinatarajiwa kutolewa katika vituo vya huduma ya pamoja vya mipakani (One stop border post).


Habari hii kama ilivyoandikwa na gazeti la siku la Mwananchi


















































































Email ThisBlogThis!Share to XShare to FacebookShare to Pinterest
Posted in Habari | No comments
Newer Post Older Post Home
View mobile version

0 comments:

Post a Comment

Subscribe to: Post Comments (Atom)

Popular Posts

  • Christiano Ronaldo and His 29 girlfriends List.
    Chr is tiano Ronaldo is famous as a great and cool football player. He play for England Manchester United Club, at age of 26 and he already...
  • Maadhimisho ya miaka 100 ya kituo cha makumbusho ya utamaduni wa Kisukuma - BUJORA Mwanza.
    Maadhimisho ya miaka 100 ya kituo cha makumbusho ya utamaduni wa Kisukuma - BUJORA Mwanza.                 Makumbusho ya  ka...
  • Tumehuzunika kidogo, Cesc Fabregas
  • Computer System Analyst Grade I (Business Analysis) – One Post - (Re-advertised) E-Government Agency (EGA
    Computer System Analyst Grade I (Business Analysis) – One Post - (Re-advertised) E-Government Agency (EGA) Date Listed: J...
  • Post: Part-time journalist
    Post: Part-time journalist Job Description Timely and accurately collecting African real-time news and then integrate the manuscript ...
  • Tempetation
    An Ivy League-educated marriage counselor who gives marital advice but finds it difficult to address issues with her own marriage.    Jur...
  • University of Dar es Salaam among top 100 Universities in Africa
    The university of Dar-es-Salaam has ranked fourth among top 100 popular universities and higher learning institutions in Africa. This is acc...
  • Admission of Diploma holders into Higher
    TANZANIA COMMISSION FOR UNIVERSITIES Admission of Diploma holders into Higher Education Institutions for the academic year 2013/2014. The T...
  • Community Relations Manager – (One Post)
    Community Relations Manager – (One Post) African Barrick Gold (ABG) Date Listed: May 15, 2013 Email Address: ...
  • Kim Kardashian awateka tena mashabiki kwa mavazi
    Kim Kardashian aliweza tena kuuteka umati waliohudhuria katika sherehe za kuchangisha fedha kwa ajili ya mfuko wa kuchangisha fedha kwa ajil...

Categories

  • Africa (1)
  • Announcement (13)
  • Biashara (17)
  • Breaking News (4)
  • Burudani (11)
  • East Africa News (19)
  • Education (12)
  • Entertainment (8)
  • Fashions (1)
  • Habari (41)
  • Health (1)
  • International News (14)
  • Jamii (11)
  • Jobs (120)
  • Latest Sports News (3)
  • Local News (59)
  • Makala (8)
  • Michezo (25)
  • Music (5)
  • News (12)
  • Scholarships (4)
  • Scholarships- Jobs (7)
  • Siasa (1)
  • Sport (64)
  • sports (18)
  • Technology (2)
  • Tetesi za Usajili (9)
  • usajili (1)

Blog Archive

  • ▼  2013 (335)
    • ►  September (9)
    • ►  August (18)
    • ►  July (23)
    • ►  June (27)
    • ▼  May (91)
      • Real Madrid yapatwa na kigugumizi
      • Parallel institutions vital to monitor tax adminis...
      • Agents told to exploit opportunities in insurance ...
      • Sida dishes out USD 10m to support agricultural gr...
      • Medical in Charge Emergency Medical Department Muh...
      • Office Administrator
      • Mourinho arudi zake Chelsea, Bale kuuzwa kwa paund...
      • Robin van Persie shows amazing skills v kids....
      • The Government has been urged to protect local in...
      • Dar es Salaam Goat Races to take part on 1st June ...
      • Jeshi lafanikiwa kudhibiti vurugu Mtwara
      • Neymar amua kuelekea Barcelona
      • Bayern Munich Mabingwa wapya wa Ulaya, Neymar aele...
      • Adnan Januzaj - Manchester United 2013
      • Dar Looks Forward to Obama's Tour
      • African Must Improve Livestock Data
      • Safari lager beer wins top Africa awards
      • Polisi kawe wabambikizia watu kesi
      • The implementation of 400 MW gas-fired power proje...
      • Kenyan celebrities at MTV All stars’ red carpert
      • HARUNA NIYONZIMA ASAINI MIAKA MIWILI YANGA SC
      • Bingwa wa Europa kuingia mojamoja Champions Ligi k...
      • Mtwara: Askari watuhumiwa kubaka, kumwua mjamzito,...
      • Kocha wa Malaga, Manuel Pellegrini kubwaga manyang...
      • Maonyesha ya 8 ya Vyuo Vikuu ya TCU yaanza rasmi j...
      • Picha za Mpambano baina ya Yanga na Simba
      • Torres kufungashiwa virago vyake dirisha la usajili
      • Zantel rewards winners of ‘Recharge and Win’ promo...
      • This week Sports on The Rumor Mill
      • Kandoro apongeza ushindi Safari Lager
      • Alex Ferguson's final Press conference
      • OMBI KWA MHE RAIS JAKAYA KIKWETE OKOA ARDHI YETU N...
      • BSL Interpreter / Tanzanian Orphanage
      • Linah, Barnaba kutimuliwa THT
      • Weigh Bridge Operators (3 Posts)
      • Administrative Assistant
      • David Beckhma hatiamye atundika daluga rasmi....
      • Sales Officers with AKIBA Commercial Bank PLC.
      • Bank Tellers Vacancy Posts
      • Community Relations Manager – (One Post)
      • Bookings and Marketing Officer
      • Vodacom na Samsung zazindua S4 nchini Tanzania
      • Angelina Jolie akatwa matiti kuzuia Saratani
      • Beckham aweka Rekodi mpya
      • Man Utd lift Premier League trophy
      • Ngono zembe ilivyokithiri barabara ya kuelekea Zambia
      • Roberto Mancini atolewa nishai na Roberto mwenzake
      • Mariah Carey - #Beautiful ft. Miguel
      • David Moyes, kocha mpya wa Mabingwa wa Uingereza a...
      • Finance Manager-ActionAid Tanzania
      • Operation Supervisors-Tanzania International Conta...
      • Monitoring and Evaluation Officer
      • Financial Controller
      • Human Resources and Administration Officer
      • Tanzania has a long bilateral relations with Arabs
      • Goat charity races to raise billions for community...
      • Youth jobs’ gains wiped out by slow recovery
      • AJIRA KWA VIJANA ZAATHIRIWA NA UKUAJI MDOGO WA UC...
      • Donors pledged Tsh 800bn in the general budget sup...
      • Sir Alex Fergsuon Angatuka MAnchester United
      • Accounts Officer
      • Accountant(s)-Vacancy
      • Human Resources and Administration Officer
      • ILO report shows why social protection is crucial ...
      • The East African Round Up
      • Afdb organizes pan-African training workshop
      • Competitive private sector a key to economic growth
      • African financial markets launch its website
      • Vodacom, GNLD signs deal to help clients
      • Nini Chanzo cha Tamaa ya Ngono
      • KAULI YA SERIKALI BUNGENI KUHUSU MLIPUKO ULIOTOKEA...
      • Huyu Ndiye Gareth Bale...
      • Mbatia ataka Kawambwa si tu ajiuzulu, bali ikiweze...
      • Workers around the globe divine on decent jobs.
      • CCM top echelons connected to illegal ivory dealing.
      • TPC set aside incentives to motivate its workers
      • TAMKO LA MTANDAO WA WATETEZI WA HAKI ZA BINADAMU (...
      • Mourinho awataka Frank Lampard na John Terry kubak...
      • Assistant F&B Manager
      • Consultant for End Term Evaluation (Tandahimba Com...
      • Accountant
      • Administration Secretary
      • Website Administrator/Customer Care
      • Marketing and Sales personnel.
      • Information Technology Manager
      • Serikali yachukua uamuzi mgumu, yafuta matokeo
      • Real Madrid wamtaka Chicharito kwa Paundi ml 25
      • Maadhimisho ya miaka 100 ya kituo cha makumbusho y...
      • Rapa wa Kriss Kross afariki Dunia jijini Atlanta
      • Discover new ideas, technologies and business oppo...
      • UFALME wA SOKA LA UHISAPNIA WAKARIBIA UKINGONI.
    • ►  April (53)
    • ►  March (41)
    • ►  February (59)
    • ►  January (14)
  • ►  2012 (162)
    • ►  December (42)
    • ►  November (70)
    • ►  October (50)
Powered by Blogger.

About Me

Unknown
View my complete profile