MAKANGALESOPHIE

  • Subscribe to our RSS feed.
  • Twitter
  • StumbleUpon
  • Reddit
  • Facebook
  • Digg

Saturday, 27 October 2012

Dk Slaa amlipua JK

Posted on 03:59 by Unknown
Mwandishi Wetu, Tabora

KATIBU Mkuu wa Chadema, Dk Willibrod Slaa amemlipua Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete akidai kuwa hana ubavu wa kupambana na rushwa kwa kuwa chama chake kiliingia madarakani kwa rushwa katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2005.

Akihutubia katika mikutano ya hadhara katika Vijiji vya Kata za Kiloleli na Ipole, wilayani Sikonge, Mkoa wa Tabora, Dk Slaa alisema rushwa inazidi kukua siku hadi siku nchini.

Alidai kwa kuwa viongozi wa CCM waliingia madarakani kwa njia ya rushwa ndiyo maana hawawezi kulimaliza tatizo hilo.

Dk Slaa alisema Rais Kikwete anatania kuhusu tatizo la rushwa kwa kuzungumza tu majukwaani, huku akiwalinda washirika wake.

Alisema kama Rais Kikwete angekuwa mkweli angewakamata wamiliki wa Kampuni ya Kagoda ambao ni watuhumiwa wa wizi wa fedha za Akaunti ya Madeni ya Nje (Epa) katika Benki Kuu ya Tanzania (BoT).

Alidai kuwa ameshindwa kuwakamata kwa sababu fedha hizo ndizo zilitumika kumwingiza madarakani katika uchaguzi wa 2005.

Katibu mkuu huyo wa Chadema alisema vitendo vya rushwa vilivyojitokeza katika uchaguzi wa viongozi wa CCM ni kielelezo tosha kwamba, chama hicho hakina uwezo tena wa kupambana na rushwa.

"Tunawaambia CCM kuwa chama chao kimeoza kuanzia juu hadi chini, sasa mafisadi wameshika hatamu ndani ya chama hicho,” alisema.

Dk Slaa alisema, “Hivi Watanzania tunahitaji ushahidi wa namna gani ili kubaini uozo katika CCM na tuungane kukiondoa madarakani.”

Aliongeza, "Wakati chama hicho kinatopea kwenye lindi la rushwa na ufisadi, kiongozi wake mkuu ambaye Rais Kikwete naye anaishia kulalamika tu.”

Slaa alisema Rais Kikwete angekuwa na nia ya dhati
katika kupambana na rushwa, angeifanyia kazi orodha ya majina 11 ya watuhumiwa wakubwa wa ufisadi iliyotolewa katika Viwanja Mwembeyanga, jijini Dar es Salaam Septemba 2007.

Alisema kuendelea kulalamikia kuhusu rushwa bila kuchukua hatua yoyote, kunawashangaza wananchi ambao wanaona hata Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) bora ingevunjwa.

Hatuwezi kukubali taifa liangamie kwa sababu Rais anashindwa kuchukua hatua dhidi ya mafisadi na wala rushwa.

Rais Kikwete

Hivi karibuni Rais Kikwete wakati akifungua Mkutano Mkuu wa UVCCM mjini Dodoma aliwaasa vijana wa chama hicho kutojihusisha na rushwa hatua ambayo inaonekana sawa na kumpigia mbuzi gitaa.

Katika hotuba yake, Kikwete aliwaambia 'watajuta', ikiwa watachagua viongozi kwa misingi ya rushwa.

“Nawaambieni, mkifanya mchezo ipo siku mtakuja kujuta maana mkishamchagua kiongozi asiyefaa, mtalazimika kuwa naye huyohuyo hadi 2017, na kama Waswahili wanavyosema majuto ni mjukuu,” alisema Kikwete.

Kauli hiyo ya Kikwete ni kama aliyoitoa wakati akiahirisha Mkutano Mkuu wa Jumuiya ya Wanawake ya chama hicho (UWT)aliposema kuwa, CCM kinakwenda kubaya kutokana na chaguzi zake kugubikwa na vitendo vya rushwa.

Kikwete alisema siku zilizopita vitendo hivyo vilikuwa vikihusishwa zaidi na wanaume, lakini akaeleza kushangazwa kwake na makundi ya kina mama nao kuanza kujihusisha na rushwa.

Msekwa alonga

Makamu Mwenyekiti wa CCM (Bara), Pius Msekwa amezidi kuwasha moto ndani ya chama hicho, baada ya kuvitaka vyombo vya dola kuwachukulia hatua za kisheria wote waliotuhumiwa na rushwa katika uchaguzi wa ndani wa chama hicho.

Kauli ya Msekwa imekuja ikiwa ni siku tatu baada ya kuwapo kwa tuhuma za rushwa kutawala ndani ya uchaguzi wa Jumuiya ya  Umoja wa Vijana( UVCCM) na ule wa Jumuiya ya Wanawake (UWT) zilizomalizika mjini Dodoma.

Hata hivyo, kauli ya Msekwa inapingana na mawazo ya makada wengi wa chama hicho wanaopinga rushwa wakisema kuwa, uongozi wa chama unapaswa kuonyesha kwa vitendo dhamira ya kweli ya kukiokoa chama hicho ambacho hata Mwenyikiti wake, Rais Jakaya Kikwete alisema; “Rushwa inatupeleka kubaya.”

Matokeo ya uchaguzi wa UVCCM ndiyo yaliyozua tafrani kubwa kiasi cha baadhi ya wajumbe wa mkutano mkuu wa jumuiya hiyo, kumsindikiza kwa mabango Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk Ali Mohamed Shein baada ya kufunga mkutano huo.

Mabango hayo yaliyokuwa na ujumbe wa kulalamikia mchakato wa uchaguzi kwamba ulitawaliwa na rushwa, yalitanguliwa na kauli za walalamikaji ambao tayari walikuwa wamewaambia waandishi wa habari kuwa wanamwomba Rais Kikwete atengue matokeo hayo, ikiwezekana katika muda wa saa 24.

Akizungumza jana asubuhi jijini Dar es Salaam, Msekwa alisema; "Kwanza nataka kusema, wote wenye malalamiko walitakiwa kuyapeleka kwenye ngazi husika, nimesikitishwa na hao ambao wamempa Rais saa 24 kufuta matokeo ya uchaguzi”.

"Hizi ni fujo tu, wapi kuna mamlaka inayomwamuru Rais au mwenyekiti kufanya hivyo, wanatakiwa kufuata taratibu na kanuni za uchaguzi... Hivi ni kifungu gani cha sheria kinachosema hivyo?," alihoji Msekwa.

Msekwa ambaye alikuwa akihojiwa na Kituo cha Radio One jana alisema kuwa kuna kanuni na taratibu mbalimbali za kuwasilisha malalamiko, ndipo hoja zinaweza kusikilizwa na kupata mafanikio.

Akizungumzia suala la rushwa ndani ya uchaguzi, alisema ni tatizo lililosambaa kwenye jamii na ni kasoro na upungufu uliokuwa sugu.

"Rushwa imesambaa kila mahali, polisi kuna rushwa, mahakamani rushwa, lazima tukemee, nimewahi kuzungumzia hili la rushwa kuwa ni kosa la jinai, lakini bado nasema kukemea haitoshi.

Waaswa kukataa mizigo mizito

Naye Mwenyekiti wa Chadema Mkoa wa Tabora, Kansa Mbarouk akiwaambia wananchi wa kata hizo kwamba ugumu wa maisha unaowakabili unatoka na sera mbaya ya chama tawala.

Mbarook alisema CCM ya Mwalimu Julius Nyerere iliyokuwa ikishughulikia matatizo ya watu sasa haipo tena, badala yake wameichukua mafisadi.

Alisema chama hicho sasa kimebaki kuwa adui wa kuminya haki za raia.

"Miaka mingi sisi tumewabeba, tena wanatumia maneno yaleyale ya ‘Mzigo mzito mpatie Mnyamwezi akubebee’. Kwa hiyo Watanzania wa Tabora kwa muda mrefu tumekuwa tukiibeba CCM wakati wenzetu mikoa mingine wameshaikataa.
Aliongeza, Sasa ni wakati mwafaka kuanza kuutua huu mzigo, umetuchosha,” alisema huku akimpigia debe mgombea wa Chadema, David William katika kinyanganyiro cha udiwani kwenye uchaguzi mdogo utakaofanyika kesho katika eneo hilo.

Chanzo Gazeti la mwananchi
Email ThisBlogThis!Share to XShare to FacebookShare to Pinterest
Posted in Local News | No comments
Newer Post Older Post Home
View mobile version

0 comments:

Post a Comment

Subscribe to: Post Comments (Atom)

Popular Posts

  • Christiano Ronaldo and His 29 girlfriends List.
    Chr is tiano Ronaldo is famous as a great and cool football player. He play for England Manchester United Club, at age of 26 and he already...
  • Maadhimisho ya miaka 100 ya kituo cha makumbusho ya utamaduni wa Kisukuma - BUJORA Mwanza.
    Maadhimisho ya miaka 100 ya kituo cha makumbusho ya utamaduni wa Kisukuma - BUJORA Mwanza.                 Makumbusho ya  ka...
  • Computer System Analyst Grade I (Business Analysis) – One Post - (Re-advertised) E-Government Agency (EGA
    Computer System Analyst Grade I (Business Analysis) – One Post - (Re-advertised) E-Government Agency (EGA) Date Listed: J...
  • Tumehuzunika kidogo, Cesc Fabregas
  • Post: Part-time journalist
    Post: Part-time journalist Job Description Timely and accurately collecting African real-time news and then integrate the manuscript ...
  • Tempetation
    An Ivy League-educated marriage counselor who gives marital advice but finds it difficult to address issues with her own marriage.    Jur...
  • University of Dar es Salaam among top 100 Universities in Africa
    The university of Dar-es-Salaam has ranked fourth among top 100 popular universities and higher learning institutions in Africa. This is acc...
  • Community Relations Manager – (One Post)
    Community Relations Manager – (One Post) African Barrick Gold (ABG) Date Listed: May 15, 2013 Email Address: ...
  • Admission of Diploma holders into Higher
    TANZANIA COMMISSION FOR UNIVERSITIES Admission of Diploma holders into Higher Education Institutions for the academic year 2013/2014. The T...
  • Kim Kardashian awateka tena mashabiki kwa mavazi
    Kim Kardashian aliweza tena kuuteka umati waliohudhuria katika sherehe za kuchangisha fedha kwa ajili ya mfuko wa kuchangisha fedha kwa ajil...

Categories

  • Africa (1)
  • Announcement (13)
  • Biashara (17)
  • Breaking News (4)
  • Burudani (11)
  • East Africa News (19)
  • Education (12)
  • Entertainment (8)
  • Fashions (1)
  • Habari (41)
  • Health (1)
  • International News (14)
  • Jamii (11)
  • Jobs (120)
  • Latest Sports News (3)
  • Local News (59)
  • Makala (8)
  • Michezo (25)
  • Music (5)
  • News (12)
  • Scholarships (4)
  • Scholarships- Jobs (7)
  • Siasa (1)
  • Sport (64)
  • sports (18)
  • Technology (2)
  • Tetesi za Usajili (9)
  • usajili (1)

Blog Archive

  • ►  2013 (335)
    • ►  September (9)
    • ►  August (18)
    • ►  July (23)
    • ►  June (27)
    • ►  May (91)
    • ►  April (53)
    • ►  March (41)
    • ►  February (59)
    • ►  January (14)
  • ▼  2012 (162)
    • ►  December (42)
    • ►  November (70)
    • ▼  October (50)
      • Hawa Jamaa hata Huruma hawana
      • World Bank report: Remove cross-border restriction...
      • Samsung:vowed to continue expanding its presence i...
      • Volunteer roles available in Tanzania
      • International Graduate Programme– Specialist Funct...
      • International Graduate Programme– Consumer Bank, S...
      • International Graduate Programme - Wholesale Bank,...
      • Consumer Bank Fast Track Programme, Standard Chart...
      • Management Accountant for Agricultural Development...
      • Twiga Cement awards Quarry Life winners
      • Barclays Bank Tanzania:Launched new Collections a...
      • Consumer Reports Auto Reliability Survey: Ford fal...
      • Blackaburn Rovers mazungumzoni na Harry Redknapp
      • Prem stars battle Messi ‘n Ron
      • TANZANIA PORTLAND CEMENT COMPANY LTD (TPCC LTD) AW...
      • The 2nd Children Arts and Cultural Festival
      • Michezo ya Ligi kuu ya Uingereza wikiendi hii kati...
      • Liverpool yalia na Simon Bennett, Chelsea yalia na...
      • Zitto: Vigogo walioficha mabilioni Uswisi kukiona
      • Di Matteo aulilia uongozi juu ya Ashley Cole!!
      • I'll talk with with Fergie - I've been a fan longe...
      • Kikongwe cha miaka 80 chamjia juu Fergie kuhusu mt...
      • Breaking: Wavaa vimini muwe macho
      • Dk Slaa amlipua JK
      • Sheikh Mubajje, Kayongo wanted out of office
      • FUBA: KIU Titans on trial against Miracle
      • Call for Applications for Journalism Training in S...
      • Trey Songz - Heart Attack
      • MAN UTD boss admits Chelsea's talented trio could ...
      • New Video: Far East Movement - Little Bird
      • MAN CITY boss has hit back at players who are not ...
      • Habari za Michezo mchanganyiko
      • Ligi ya mabingwa msimu ni Balaaa
      • Christiano Ronaldo and His 29 girlfriends List.
      • Mwanadada Jprdana atemana rasmi na mchumba wake
      • Barcelona vs Celtic 2-1 All Goals and Highlights 1...
      • Manchester United vs Sporting Braga [3-2] All Goal...
      • Je mwisho wa Barcelona ndio umefika
      • Rais Kikwete afungua mkutano mkuu wa 8 wa UVCCM .
      • Kim Kardashian awateka tena mashabiki kwa mavazi
      • Karaoke Night.
      • Reservations & Marketing For Africa-Vacancy
      • Marketing Officers (3posts)
      • Internship Placement
      • Regional and District Coordinators
      • John Terry katika kuongoza kampeni ya kupinga Ubag...
      • Italian scientists convicted over earthquake warning
      • Jalada la Elizabeth Michael ‘Lulu’ larejeshwa Kisu...
      • Wakristo Geita wasema OLE! Vitisho, uharibifu wa m...
      • Fergie: I'm not teed off with shirt snub Rio ReAl...
Powered by Blogger.

About Me

Unknown
View my complete profile